The House of Favourite Newspapers

Muna: Lulu Ananinyima Usingizi!

0
Rose Alphonce ‘Muna’

MSANII wa filamu na mjasiriamali, Rose Alphonce ‘Muna’ amesema kuwa, anapitia katika kipindi kigumu sana cha kumuuguza mtoto wake lakini muda huohuo kukosa usingizi kutokana na kesi inayoendelea ya mdogo wake wa hiari, Elizabeth Michael ‘Lulu’.

Akizungumza na Star Mix, Muna ambaye tangu kesi ya Lulu imeanza kusikilizwa hakosi kuwa naye mahakamani alisema, amekuwa kwenye kipindi kigumu kwa kuwa takribani miezi miwili anamuuguza mtoto wake mguu wenye majeraha lakini pia hapati usingizi kwa ajili ya kesi ya Lulu.

 

“Yaani najiona kabisa kama huu mwaka ni wangu, maana pale Muhimbili walishanizoea kabisa, nimekaa muda mrefu nikimuuguza mwanangu mguu lakini ukiachana na hilo nahangaika na upande wa pili ishu ya Lulu mpaka nachanganyikiwa,” alisema Muna.

 

STORI: IMELDA MTEMA

Leave A Reply