Muonekano wa Dar Live Yatakapofanyika Mapambano ya Ngumi Usiku wa Leo
Matayarisho ya mapambano ya ngumi ya Afrika Mashariki na Kati yaliyoandaliwa na Global TV Online katika Ukumbi wa Dar Live Mbagala-Zakhem, jijini Dar es Salaam yamekamilika na kinachongojewa kwa sasa ni wadau mbalimbali walioalikwa kuingia ukumbini hapo kuanzia sasa. Mapambano hayo yataonyeshwa mubashara (live) kuanzia saa 2:00 usiku leo.
Mapambano hayo ambayo yatarushwa mubashara na Televisheni ya Mtandaoni ya Global TV Online BURE, yatakuwa kama ifuatavyo:
CHICHI MAWE VS ISRAEL KAMWAMBA
NASIBU RAMADHAN VS BERNARD MWANGO
IDD PIALALI (TANZANIA) VS REGION CHAMPION (MALAWI)
Subscribe hapa www.youtube.com/user/uwazi1