Mwanaharakati wa masuala ya siasa, Cyprian Musiba ameibuka na kujibu hoja ya Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini (CHADEMA), aliyoiwasilisha bungeni juu yake kuwa alisema ataua.
Musiba amekanusha tuhuma hizo kwa kusema kwamba hajawai kusema atamuua mtu yeyote yule isipokuwa alisema kama angekuwa IGP wa nchi hii basi angemuweka mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, miaka 200 jela.
Aidha Musiba amesema Mbunge Selasini, alimuambia kuwa ana mpango wa kutoka Chadema na kuhamia CCM, na pia ameendelea kusisitiza kuwa Rais Magufuli na serikali iliyopo madarakani ni lazima iheshimiwe.
Comments are closed.