The House of Favourite Newspapers

Mwakinyo, Tony Rashid Ulingoni Septemba 3

0

MABONDIA wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo na Tonny Rashid, watatarajia kupanda ulingoni Septemba 3, mwaka huu kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar.

 

Mwakinyo ambaye ni bingwa wa Afrika ‘ABU’ atapanda ulingoni dhidi ya Julius Indongo kutoka Namibia katika Pambano la Mabingwa wa Ulingo, wakati Tonny Rashid akitarajia kupanda ulingoni na Bongani Mahlangu wa Afrika Kusini.

 

Akizungumza na Spoti Xtra, promota wa pambano hilo kutoka Amoma Promotion, Amos Nkondo, alisema sababu kubwa ya kuandaa pambano hilo ambalo litahusisha mabondia wa kimataifa ni kutaka kukata kiu ya mashabiki wa ngumi nchini.

 

“Hili pambano kubwa ambalo litahusisha mabingwa wawili, Hassan Mwakinyo na Tonny Rashid ambao watatetea mikanda yao ya ubingwa dhidi ya mabondia kutoka Afrika Kusini na Namibia ili kuleta msisimko halisi wa ngumi na kutaka kukata kiu ya mashabiki.

 

Tumeamua kusimamisha pambano hili kwa kushirikiana na wenzetu wa Mwakinyo Pro tofauti na ilivyozoeleka kwa sababu tunaona muda muafaka kwa wapenzi wa ngumi kuungana pamoja na kufanya mambo makubwa kwa maslahi mapana ya mabondia,” alisema Amoma.

 

Mabondia wengine watakaopanda ulingoni ni Allen Kabungo dhidi ya Haidari Mchanjo, Manyi Issa na Adam Yusuph, wakati Abdul Juma atacheza na Ally Ngwando, Flora Malechela atazichapa na Aisha Kizengo, huku Ayoub Salim akitarajia kucheza na Rashid Kazumba.

MWANDISHI WETU,Dar es Salaam

Leave A Reply