The House of Favourite Newspapers

Mwambusi Ana Dk 360 za Kuishangaza Simba

0

 JUMA Mwambusi, Kaimu Kocha Mkuu wa Yanga, ana takribani dakika 360 kusaka pointi 12, kabla ya kukutana na Simba katika Dabi ya Kariakoo.

 

Mechi nne ambazo ni sawa na dakika 360 ndani ya Aprili kwa Yanga, zitaanzia Aprili 10 dhidi ya KMC, Uwanja wa Mkapa.

Mchezo wa kwanza walipokutana CCM Kirumba, Mwanza, ubao ulisoma KMC 1-2 Yanga.Aprili 17, Yanga itasaka pointi tatu mbele ya Biashara United, Uwanja wa Mkapa, mchezo wa kwanza walipokutana Karume, Mara, ubao ulisoma Biashara United 0-1 Yanga.

 

Baada ya hapo, Aprili 20, Yanga itamenyana na Gwambina FC, Uwanja wa Mkapa, zilipokutana Gwambina Complex, ngoma ilikamilika 0-0.

Aprili 25, Yanga itasaka ushindi mbele ya Azam FC, Uwanja wa Mkapa, mchezo wa kwanza walipokutana Azam Complex, ubao ulisoma Azam FC 0-1 Yanga.

 

Baada ya kumaliza vigongo hivyo katika dakika 360 kwenye ligi, kigongo chake kinachofuata Mei 8, Uwanja wa Mkapa, dhidi ya mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Simba ampapo walipokutana mechi ya kwanza uwanjani hapo, ubao ulisoma Yanga 1-1 Simba.

Kwenye msimamo wa ligi hivi sasa, Yanga ipo nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 50 baada ya kucheza mechi 23, Simba wapo nafasi ya pili na pointi 46 baada ya kucheza mechi 20.Endapo Mwambusi atafanya vizuri katika mechi hizo nne, ni wazi atakuwa anakwenda kupambana na Simba huku wapinzani wao wakiwa na tahadhari kubwa.

STORI: LUNYAMADZO MLYUKA, DAR ES SALAAM

Leave A Reply