The House of Favourite Newspapers

Mwamnyeto Kumsalimia Mara Mbilimbili Onyango

0

BEKI wa kati wa Yanga, Bakari Mwamnyeto, akimuona Joash Onyango wa Simba, atalazimika kumsalimia mara mbilimbili kwa kuwa amempoteza jumlajumla kwenye kuweka lango salama ndani ya uwanja licha ya kutumia muda mfupi uwanjani.

 

 

Mechi 21 ambazo Yanga imecheza, Mwamnyeto ameanza mechi 20 na kuyeyusha dakika zote 90, hivyo uwanjani ametumia jumla ya dakika 1,800 na kushuhudia timu yake ikiokota nyavuni mabao 11. Ana wastani wa kuokota bao moja nyavuni kila baada ya dakika 163.

 

 

Onyango kwenye mechi 18 ambazo Simba wamecheza, yeye amecheza jumla ya mechi 15 na ni mechi 14 ameyeyusha dakika 90 na kumfanya atumie dakika 1,260 na ameshuhudia timu yake ikiokota nyavuni mabao 8. Ana wastani wa kuokota bao moja kila baada ya dakika 157.

 

 

Onyango mchezo mmoja alitumia dakika 68 na kumfanya jumla kwenye mechi 15 atumie dakika 1,328 ambapo amefunga bao moja na kuonyeshwa kadi moja ya njano.

 

 

Za Mwamnyeto ni hizi hapa:- Tanzania Prisons 90, Mbeya City 90, Kagera Sugar 90, Mtibwa Sugar 90, Coastal Union 90, Polisi Tanzania 90, KMC 90, Biashara United 90, Simba 90, Namungo 90 njano moja, Azam FC 90, JKT Tanzania 90, Ruvu Shooting 90, Mwadui 90, Dodoma 90, Ihefu 90, Prisons 90, Mbeya City 90, Kagera Sugar 90, Mtibwa Sugar 90.

 

 

Za Onyango:- Ihefu 90, Mtibwa Sugar 90, Biashara United 90, Gwambina 90, JKT Tanzania 90, Prisons 90, Ruvu Shooting 90, Mwadui 90, Kagera Sugar 90, Yanga 90, Coastal Union 68, Polisi Tanzania 90, Mbeya City 90, Ihefu 90, Biashara United 90, njano moja.

Lunyamadzo Mlyuka, Dar es Salaam

Leave A Reply