The House of Favourite Newspapers

MWANANCHI KINONDONI ALILIA MSAADA WA MAKONDA

Mkazi wa  Wilaya ya Kinondoni,  Ally  Abdallah akizungumza na waandishi wa habari.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kinondoni, Mussa Embe, akitoa ufafanuzi juu ya mgogoro huo.
.…Akiwa na baadhi ya ndugu zake wakionyesha baadhi ya nyaraka kwa waandishi wa habari (hawapo pichana)

 

BAADA Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam,  Paul Makonda, kushughulikia kero mbalimbali za migogoro ya ardhi na kutolea ufumbuzi, tatizo hilo bado linaendelea kwa baadhi ya watu ambao wanaenda kinyume na taratibu zilizopo.

 

Hayo yamebainika baada ya mwananchi mmoja anayefahamika  kwa jina la  Ally  Abdallah  ambaye ni mmiliki wa kiwanja  namba 212 kilichopo Kinondoni, Mkwajuni,   kujitokeza mbele ya vyombo vya habari kulalamikia kuwa  nyumba yake imetapeliwa na  mtu aliyemtaja kwa jina la Suleiman  ambaye naye amekuwa akidai ni mmiliki halali wa kiwanja hicho

 

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Ally alisema kuwa yeye ndiye mmiliki halali wa eneo hilo na akaonyesha nyaraka mbalimbali kwa waandishi wa habari  za barua ambazo alipewa kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam  zinazoonyesha kuwa  namba ya kiwanja anayoitumia inampa uhalali kuwa yeye ndiye mmiliki wa eneo hilo.

Baada ya maelezo hayo waandishi wa habari walizungumza na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kinondoni, Mussa Embe,  ambaye alikiri kuufahamu mgogoro huo na kusema kuwa yeye anatambua  eneo lake halina kiwanja namba 1200 kama mlalamikiwa anavyodai  na badala yake eneo la kiwanja chake mwisho ni 429.

Abdallah amemwomba Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi na Mkuu wa Mkoa kuingilia kati mgogoro huo ili  haki ipatikane.

 

 

 

Comments are closed.