Mwarabu Kutembea na Sarah Wake, Harmonize Kajibu – Video
MSANII wa Bongo Fleva, Harmonize amefunguka kuhusu tetesi za mpenzi wake, Sarah kutoka kimapenzi na Bodigadi wa Diamond Platinumz, Mwarabu Fighter na kusema anaheshimiana sana na Bodigadi huyo ambaye amedai ni kama kaka yake, hivyo hawawezi kuingia katika ugomvi kisa mwanamke.
Akizungumza wakati wa mahojiano kwenye Shoo ya Mbosso iliyofanyika usiku wa kuamkia leo, harmonize alisema mpenzi wake (Sarah) siyo malaika, kwani anawezakutongozwa na mwanamme yeyote.
Comments are closed.