Mwili wa mzee John Alfonso Nchimbi ambaye ni baba wa Balozi Emmanuel Nchimbi aliyefariki dunia Januari 23, 2022 katika Hospitali ya JKCI, umeagwa rasmi kwenye ibada iliyofanyika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Pio jijini Dar es Salaam na kuzikwa katika makaburi ya Kinondoni, leo Jumanne, Januari 25, 2022 ambapo katika maziko hayo amepigiwa mizinga 10 ya heshima ya kijeshi.