MWILI WA MAREHEMU RUGE UMEWASILI NCHINI
Mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media, Ruge Mutahaba umewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ukitokea Afrika Kusini alikokuwa akipatiwa matibabu. Sasa ni safari ya kuelekea Hospitali ya Lugalo kwa ajili ya kuhifadhiwa kabla ya taratibu za kuagwa kesho. Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda alikuwa mmoja wa watu waliofika kuupokea mwili huo.
PICHA: DENIS MTIMA | GPL
Comments are closed.