MWINGINE KUTOKA MBEYA ASHINDA BEATS BY DRE ZA SPOTI XTRA
MSHINDI wa shindano la Gazeti la michezo la Spoti Xtra la kuwania headphones za Beats by Dre, Mwinyi Twaha, mkazi wa Mbeya, amekabidhiwa zawadi yake hiyo leo Jumatatu katika ofisi za Global Publishers zilizopo Sinza Mori jijini Dar es Salaam
Mdogo wake, Fadhili Mwinyi ndio alipokea zawadi hiyo kwa niaba yake na kuwahamasisha wasomaji wa gazeti la Spoti Xtra kushiriki shindano hilo kwani zawadi ni za uhakika.
Pamoja na shindano la headphones za Beats by Dre lakini pia gazeti la Spoti Xtra linalotoka kila Jumapili linaendesha shindano la kutoa jezi za timu za Ligi Kuu England.
Comments are closed.