The House of Favourite Newspapers

Mzee Mbizo Aingia Studio Kupiga Kolabo na Mwanaye

INAWEZA kukuwia vigumu kuamini, lakini ndiyo hivyo tena, akiwa anatimiza umri wa miaka 68, miaka 39 ya kuwepo kwenye fani za michezo na burudani, hatimaye Mzee Juma Mbizo ameamua kuingia studio kwa mara kwanza na kufanya ‘kolabo’ na mwanae H-Mbizo.

 

Naam Mzee Mbizo amejitosa katika studio za Fire Music chini producer More Fire na kurekodi wimbo wa pamoja na H-Mbizo aliyepata kutamba na wimbo wa “Mchumba”.

 

H-Mbizo ambaye pia mwandishi mzuri wa nyimbo akiwa amewaandikia wasanii wengi akiwemo Snura kupitia wimbo “Majanga”, ameuambia mtandao huu kuwa kibao hicho alichoimba na baba yake kitaachiwa hewani mwezi huu.

Licha ya ukongwe wake kwenye game na utalaam wa kuandaa matamasha makubwa ya burudani, lakini Mzee Mbizo hakuwahi kuingia studio na kurekodi wimbo wowote ule na hii ndio hali itayofanya kazi hii alishoshirikishwa na mwanae iteke masikio ya mashabiki wengi wa muziki.

Comments are closed.