INATIA HURUMA! Zikiwa zimepita siku kumi tangu apate pigo la kufiwa na mkewe mdogo, Chiku Khamis, aliyekuwa Mfalme wa Taarab Bongo na Mkurugenzi wa Kundi la Jahazi Modern, Alhaj Mzee Yusuf amefunguka kuhusu bifu kati ya mkewe mkubwa Leila Rashid na dada yake Khadija Yusuf.
Risasi Mchanganyiko lilipotaka kujua kama amelifanyia kazi bifu la mkewe huyo na dada yake Khadija Yusuf, alifunguka kuwa bado kwa sababu kichwa chake hakiko sawasawa.
“Kichwa changu hakijakaa sawa bado, mpaka niweze kushughulikia mambo ya watu, wale ni watu wazima, wanatakiwa wajisuluhishe wenyewe halafu mimi nitakuja kusaidia baadaye nikiwa sawa,” alisema Mzee Yusuf.