The House of Favourite Newspapers

Mzungu ‘Mtata’ Aendelea Kusota Rumande (VIDEO)

0
Menelaos Tsampos.

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo Agosti 18, 2017 imemnyima dhamana raia wa Afrika Kusini ambaye ni mhandisi, Menelaos Tsampos, anayetuhumiwa kwa kosa la kumtishia mtu kwa njia ya mtandao kupitia mfumo wa kompyuta.

Upande wa utetezi unaoongozwa na wakili Deus Singa ulikuwa ukiiomba mahakama hiyo kumpa dhamana Menelaos wakati kesi yake ikiendelea, huku upande wa mashitaka ukipinga kupewa dhamana kwa kile walichokieleza kuwa akiachiwa huru anaweza kumdhuru aliyemtishia maisha.

Kutokana na hoja hizo, hakimu aliiahirisha kesi hiyo hadi kesho Agosti 18, 2017 ambapo itaelezwa iwapo atapewa dhamana. Mshitakiwa wamerudishwa rumande.

Menelaos anadaiwa mahakamani hapo kuwa Juni 22, mwaka huu maeneo ya jijini Dar es Salaam, kupitia mfumo wa kompyuta alituma ujumbe wa baruapepe (E-mail) uliokuwa na maneno ya vitisho kwa mtu anayeitwa Costa Gianna, ikiwa ni kinyume na sheria ya mtandao kifungu cha 23(1) na (2) namba 14 ya mwaka 2015.

Mzungu huyo amekua gumzo mahakamani hapo alipoanzisha timbwili kortini hapo juzi baada ya kuwachimba mkwara mzito waandishi wa habari waliokuwa wakimpiga picha siku ya kwanza alipofikishwa mahakamani.

Dhamana ya Mzungu Aliyeleta Timbwili Mahakamani Yadunda, Aendelea Kusota

Leave A Reply