The House of Favourite Newspapers

Nafasi Mpya za Kazi Serikalini

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inawahimiza Watanzania wenye sifa kuomba nafasi za ajira katika Sekretarieti ya Jumuiya ya Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) yenye makao makuu Bujumbura, Burundi; Kituo cha Kikanda cha Kupambana na Ukatili na Unyanyasaji wa Kijinsia (Regional Training Facility on SGBV) kilichopo Kampala, Uganda na Kituo cha Demokrasia na Utawala Bora cha Levy Mwanawasa (Levy Mwanawsa Regional Centre for Democracy and Good Governance) kilichopo Lusaka, Zambia.

Ajira hizo ni kama ifuatavyo:-

SEKRETARIETI YA MAZIWA MAKUU

  1. Mkurugenzi wa Utawala na Fedha (Director, Administration and Finance);Mkurugenzi wa Nyaraka na Mikutano (Director, Documentation and Conferences);
  2. Mkurugenzi wa Mawasiliano (Director, Communications);
  3. Mshauri wa Masuala ya Sheria (Legal Adviser).
KITUO CHA DEMOKRASIA NA UTAWALA BORA CHA LEVY MWANAWASA
  1. Mkurugenzi wa Kanda (Regional Director);
  2. Mkuu wa Utafiti (Head, Research);
  3. Mkuu wa Jukwaa na Uchunguzi (Head, Fora and Observatories)
KITUO CHA KIKANDA CHA KUPAMBANA NA UKATILI NA UNYANYASAJI WA KIJINSIA
  1. Mratibu wa Mafunzo (Training Coordinator) na
  2. Mratibu wa masuala ya TEHAMA, Utafiti na Elimu (IT, Research and Knowledge Coordinator).

Waombaji wa nafasi hizo wanapaswa kuwasilisha barua za maombi katika Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kabla ya tarehe 4 Aprili 2019 ili yaweze kuwasilishwa kwenye Sekretarieti ya ICGLR kwa wakati.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma
25 Machi 2019

Comments are closed.