Nafasi Mpya za Kazi Serikalini
Ajira hizo ni kama ifuatavyo:-
SEKRETARIETI YA MAZIWA MAKUU
- Mkurugenzi wa Utawala na Fedha (Director, Administration and Finance);Mkurugenzi wa Nyaraka na Mikutano (Director, Documentation and Conferences);
- Mkurugenzi wa Mawasiliano (Director, Communications);
- Mshauri wa Masuala ya Sheria (Legal Adviser).
- Mkurugenzi wa Kanda (Regional Director);
- Mkuu wa Utafiti (Head, Research);
- Mkuu wa Jukwaa na Uchunguzi (Head, Fora and Observatories)
- Mratibu wa Mafunzo (Training Coordinator) na
- Mratibu wa masuala ya TEHAMA, Utafiti na Elimu (IT, Research and Knowledge Coordinator).
Waombaji wa nafasi hizo wanapaswa kuwasilisha barua za maombi katika Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kabla ya tarehe 4 Aprili 2019 ili yaweze kuwasilishwa kwenye Sekretarieti ya ICGLR kwa wakati.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma
25 Machi 2019
Comments are closed.