The House of Favourite Newspapers

NAFASI ZA KAZI 17 MHIFADHI WANYAMAPORI III

 

OFISI ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imetangaza nafasi za kazi  17 katika Ministry of Natural Resources and Tourism. Mwisho wa kuomba kazi hizo ni 2019-02-22.

Employer: Ministry of Natural Resources and Tourism
Date Published: 2018-11-23
Application Deadline: 2019-02-22

DUTIES AND RESPONSIBILITIES:

i.Kufanya doria ndani na nje ya maeneo ya hifadhi;

ii.Kudhibiti vitendo vya ujangili nje na ndani ya hifadhi;

iii.Kusimamia shughuli za uwindaji wa kitalii na utalii wa picha;

iv.Kulinda binadamu na mali zake dhidi ya Wanyamapori;

v.Kukusanya na kulinda Nyara za Serikali;

vi.Kufanya usafi na ulinzi wa kambi;

vii.Kusimamia uingiaji na utokaji wa watu na mali zao kwenye hifadhi;

viii.Kukusanya na kutunza vielelezo vya ushahidi na kutoa ushahidi Mahakamani;

ix.Kukagua wanyamapori kwenye mashamba na mazizi ya wanyamapori na kukusanya takwimu zao;

x.Kusimamia taratibu za kusafirisha wanyamapori hai na nyara nje na ndani ya Nchi;

xi.Kudhibiti wanyamapori waharibifu;

xii.Kudhibiti moto kwenye hifadhi; na

xiii.Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa zinazoendana na taaluma yake.

 

QUALIFICATION AND EXPERIENCE:

Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha IV au kidato cha VI wenye Astashahada ya Uhifadhi Wanyamapori (Technician Certificate in Wildlife Management) kutoka Chuo cha Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi au chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.

 

REMUNERATION: Salary Scale TGS B2,.

Login to Apply

Comments are closed.