The House of Favourite Newspapers

Nahodha wa Ghana Andre Ayew kujiunga na Al Sadd SC ya Qatar

0

Nahodha wa timu ya soka ya Ghana Andre Andreyeye yuko tayari kusaini makubaliano na klabu ya Qatar Al Sadd SC. Klabu hiyo inasema imefikia makubaliano ya kumsaini nahodha huyo wa Black Stars.

 

Kijana huyo wa miaka 31 anasafiri kwenda Qatar kukamilisha kusaini mkataba.Ayew anatarajiwa huko Doha Alhamisi (leo) kufanyiwa matibabu na baadaye kutia saini makubaliano hayo.

 

Ayew amekuwa hana kilabu baada ya kandarasi yake ya miaka mitatu na klabu ya Wales Swansea City kukosa kuongezwa mwishoni mwa msimu uliopita. Ilikuja wakati klabu ilikosa kupanda hadi Ligi ya Premia dhidi ya Brentford katika fainali ya mchujo.Ripoti zinaonyesha kuwa tapata zaidi ya dola laki mbili ($ 200, 0000) kwa wiki.

 

Uhamaji wake ni sawa na mtangulizi wake kama nahodha wa Ghana Asamoah Gyan ambaye aliacha ligi ya Uingereza na kucheza Mashariki ya Kati wakati alihama kutoka Sunderland kwenda Al Ain huko UAE.

Leave A Reply