The House of Favourite Newspapers

Najua tu, Kuna Watu Wameroga

0

CHEKA NA KITIME WA GLOBAL PUBLISHERS

YAANI mi naona nina kamkosi fulani, toka nizaliwe sijawahi kupata mrembo wa nguvu. Yaani kila mara inatokea ishu ya kuniwekea kipingamizi cha kupata mrembo ambaye ana mvuto wa pekee.

Yaani naona wazi kuna mkono wa mtu. Kuna watu sijui roho zao zikoje, wao wanapenda kuona mtu anateseka hata kama wao hawapati kitu, yaani ni roho mbaya tu inamfanya mtu anakuwekea kagundu fulani basi warembo unapishana nao, wanakupita hivi hivi mubashara hawakuoni kabisa hata uwe umevaa nini.

Kwa upande wangu na hili gundu limeanza miaka mingi sana, kwanza nilikuwa sijalistukia, lakini sasa nimeshajua mambo sio sawa, kuna haja ya kutafuta mtaalamu, nisafi she nyota. Nyenzo moja muhimu sana ukitaka kupata warembo wa ukweli ni kuwa na simu inayoenda na wakati. Nimegundua kuna mtu kachafua

Nimegundua kuna mtu kachafua nyota yangu ya kupata simu kali. Unaweza kucheka lakini hilo ndilo gundu nililorogezewa, nyota ya kupata…

nyota yangu ya kupata simu kali. Unaweza kucheka lakini hilo ndilo gundu nililorogezewa, nyota ya kupata simu za kisasa imefukiwa kaburini. Warembo wa ukweli wanamaindi sana aina ya simu uliyonayo, sasa mimi nimefanyiwa kitu, kila mara nakuwa sina simu inayoenda na wakati.

Enzi zile wakati simu za twanga pepeta zinatamba, mi nilikuwa sina simu kabisa, warembo wote wa ukweli walinikataa sababu hiyo. Nikahangaika nikaja kupata kasimu kangu ka twanga pepeta, kumbe warembo wamehama wanataka watu wenye blek beri, kila ninaye jaribu kumuingia akishagundua nina twanga pepeta ananitolea nje tena kwa kashfa.

Nikajinyima nikaja kupata blek beri yangu, nikawa nairingishia hata kujaribu kuwaonyesha, warembo kila nilipowakuta, baada ya muda  nikagundua wananicheka kumbe wajanja walishahamia simu nyingine, watu wakawa wanakutana WhatsApp sijui Insta, mie nikawa siko huko, basi nikachakalika nikapata na mie simu yenye WhatsApp, ile naanza kujisifu nakuta wameanza kutumia simu za kupangusa.

Nimestrago nimepata ya kupangusa hawaniangalii mpaka nipate iphone, jamani nina mkosi gani? Sasa kununua iphone ni mtihani, nikijinyima sana naweza nikawa na iphone  mwisho wa mwaka , lakini najua tu staili nyingine ya simu itakuwa imeanza, siku nikimjua aliyeniroga namtoa kongosho!

 

Leave A Reply