The House of Favourite Newspapers

Namna rahisi na salama ya kupunguza unene

0

Ukizungumza na watu wengi wanene wanataka kujua njia ya kupunguza mafuta tumboni. Njia rahisi na salama ya kupunguza mafuta katika tumbo au kitambi ni ile ya kupangilia chakula na kufanya mazoezi.

Kama unataka kupunguza tumbo kwa haraka basi punguza kula vyakula vyenye wanga na badala yake tumia mbogamboga na matunda kwa wingi.

Vyakula kama viazi mviringo, wali, mkate hukaa tumboni kwa zaidi ya siku tatu, pia ulaji wa nyama nyekundu unasababisha kuongezeka uzito na pia huongeza ukubwa wa tumbo.

Vyakula hivyo vinatakiwa kutumiwa kwa kiasi kidogo sana. Kuna wakati tumbo linajitokeza na kuwa kubwa kuliko kawaida hali hiyo inasababishwa na kula vyakula vya wanga kwa wingi, kutokunywa maji ya kutosha na pia kula bila ya mpangilio maalum.
Vyakula vya wanga na mafuta hufanya mtu kunenepa, acha au kupunguza kula vyakula hivyo.

Tumbo kuwa kubwa ni dalili kuwa chakula unachokula hakifanyi kazi inayotakiwa, kumekuwa na ziada mwilini na hii ziada inafanyika mafuta ambayo hujiwekesha akiba katika maeneo mbalimbali ya mwili.

Kwa kuwa chakula hiki cha ziada huwa hakitakiwi, mwili hukibadilisha na kuweka akiba katika mfumo wa mafuta kitaalam kama glycogem.

Unaweza kukabiliana na kuzidi kwa protini zinazoyeyushwa na kuwekwa katika akiba kwa mfumo huo wa mafuta. Mtu mwenye tatizo hilo ni bora akapangilia mlo wake kwa siku kama ifuatavyo.

Asubuhi pata kifungua kinywa kilichokamilika, pata mlo wa mchana kama kawaida na usiku kula matunda tu kunaweza kufanya mwili wako uwe katika hali inayotakiwa.

Watu wengi wanatumia chakula cha wanga mwingi wakati wa usiku, muda ambao wanakwenda kulala na ziada ya chakula haifanyi kazi vizuri zaidi ya kujikusanya, kujibadilisha na kuhifadhiwa katika maeneo mbalimbali ya mwili hasa tumboni na kwenye makalio.

Mazoezi ya viungo husaidia kuchoma mafuta ya ziada katika mwili. Wanaume huwa na asilimia 8 hadi 20 ya mafuta katika mwili na wanawake ni asilimia 13 hadi 25.

Unapofanya mazoezi ya viungo unaongeza hewa ya oksijeni katika mapafu na wakati huohuo mwili nao unaunguza mafuta ili kutoa nguvu kwa mwili. Kwa ushauri zaidi wasiliana na daktari.

Leave A Reply