The House of Favourite Newspapers

NANDY AZINDUA BIDHAA ZAKE MWANZA, ATOA FURSA KWA VIJANA

Msanii wa kizazi kipya, Faustina Mfinanga ’Nandy akizungumza jambo.
Nandy akionyesha bidha zake.
Mmoja wa mawakala wake wa mkoa wa Mwanza naye akizungumza jambo.
Wakionyesha bidhaa hizo.

 

 

MSANII wa kizazi kipya, Faustina Mfinanga ’Nandy’amezindua bidhaa zake jijini Mwanza huku akiwataka vijana kuchangamk-ia fursa za kuzisambaza bidhaa hizo.

 

 

Bidhaa hizo zinajulikana kama’Nandy Beaty Product’ ambazo ni za aina mbili yaani ‘Nandy Beautyjelly’ (Mafuta ya kupakaa) na Nandy Beauty Soap (Sabuni za kuogea ambazo alisema kuwa zote bihaa hizo zinato katika familia ya Zoazoa.

 

 

Akizungumza na waandishi wa habari Nandy amesema kuwa bidhaa hizo zitapatikana maduka yote nchini.

Pia ametoa fursa kwa vijana wanaohitaji kusambaza bidhaa hizo kujitokeza ili kujipatia ajira pamoja na kuchangia pato la chumi wa taifa na kuomba watanzania kununua bidhaa hizo ili kukuza uchumi wa nyumbani.

 

 

“Haikuwa kazi rahisi kuona kama hii ni frsa, lakini siku moja nilikutana na Dkt. Elizabeth Kilili (GraceProdct) nikamuelezea juu ya wazo la kuanzisha biashara ya mafuta ya kujipaka na bidhaa nyingine za urembo, ndipo alinikaribisha tuwe kama Bisiness Partners katika biashara hii na niliona ni wazo zuri kwangu kwa kushirikiana naye”, alisema Nandy.

 

 

NA:DENIS MTIMA

Comments are closed.