The House of Favourite Newspapers

NAPE: Huu ni Mtihani Mkubwa kwa Serikali ya Awamu ya Tano – Video

MBUNGE wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye, akichangia hoja katika bajeti ya Wizara ya Kilimo amesema bajeti hiyo haitoshi ikilinganishwa na uhitaji halisi ili kuinua kilimo ambacho kinatoa ajira kubwa kwa wananchi hapa nchini.

 

Akitoa maoni yake Bungeni Mjini Dodoma, Nape ameishauri Serikali kupitia Wizara ya Kilimo inayoongozwa na Dkt. Charles Tizeba kurudia kuipitia na kuipanga upya bajeti hiyo ili kuiongeza iweze kuwasaidia wakulima na sekta nzima ya kilimo kwani bajeti hiyo imekuwa ikishuka kila mwaka badala ya kuongezeka hivyo kukosa uhalisia wa kuinua kilimo na wakulima.

MSIKIE NAPE AKIFUNGUKA

Comments are closed.