Navy Kenzo waapa kumuangusha Diamond Platnumz
Aika na Nahreel ‘Navy Kenzo’
Stori:Boniphace Ngumije
KUNDI la Muziki wa Bongo Fleva linaloundwa na wapendanao wawili, Aika na Nahreel ‘Navy Kenzo’ limefunguka kuwa moja ya mipango yake ya kikazi kwa sasa ni kuhakikisha linashindana kibiashara na mkali wa muziki nchini Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na ikiwezekana hata kumshinda kupitia lebo yao ya The Industry.
Akichonga na gazeti hili, mama kijacho Aika alisema kuwa anachokifanya Diamond kupitia lebo yake ya Wasafi, kukuza wasanii ni kitu kizuri lakini hata hivyo kwa upande wao kutokana na aina ya wasanii walionao kwenye lebo yao akiwemo Roseline Mohagachi ‘Seline’ aliyetoa wimbo mpya uitwao Njoo wana imani watampita Diamond.
“Tumejipanga, ukiangalia aina ya wasanii tulionao na namna wanavyoufahamu muziki utakubali kuwa tunasonga mbele, ukweli ni kwamba Diamond asipoangalia tutamkalisha chini,” alisema Aika.
KUNUNUA NA KUSOMA MAGAZETI YA GLOBAL PUBLISHERS ONLINE, INGIA HAPA==>VODACOM M-PAPER APP
*********
JIUNGE NA SOCIAL MEDIA ZETU
KWA HABARI ZA KITAIFA, KIMATAIFA, MASTAA NA MIKASA YA KUSISIMUA
INSTAGRAM: @Globalpublishers
ERIC SHIGONGO INSTAGRAM: @ericshigongo
TWITTER: @GlobalHabari
FACEBOOK: @GlobalPublishers
SUBSCRIBE YOU TUBE: Global TV Online
GLOBAL TV ONLINE: www.globaltvtz.com
HADITHI ZA KUSISIMUA NA MBINU ZA UJASIRIAMALI, ERIC SHIGONGO FACEBOOK PAGE:@shigongotz