Nay amfungukia Miss Tanzania
Nay wa Mitego.
Gladness Mallya
BAADA ya tetesi kuzagaa kuwa staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ anatoka kimapenzi na Miss Tanzania 2014, Lilian Kamazima, ameibuka na kufungukia ishu hiyo.
Lilian Kamazima
Nay wa Mitego aliiambia Risasi Vibes kuwa tetesi hizo siyo za kweli, bali huwa anampenda tu msichana huyo kutokana na muonekano wake mzuri, lakini siyo kimapenzi.
“Lilian ni mshkaji wangu tu, nampenda jinsi alivyo, sina uhusiano naye wa kimapenzi, nisije kumwaribia bure kwa mtu wake,” alisema.