The House of Favourite Newspapers

NBC Yaendelea Kusaidia Ujenzi wa Shule na Ofisi za Walimu Nchini

Meneja wa Benki ya NBC Zanzibar, Ramadhani Lesso (wa nne kushoto), akishikana mikono na Mkuu wa Mkoa Kusini Unguja, Hassan Khatibu Hassan wakati akimkabidhi msaada wa mabati  140 pamoja na vifaa vingine vya kuezekea vyenye thamani ya zaidi ya shilingi  milioni 8 kuezekea madarasa manne pamoja na ofisi mbili za walimu za shule ya Maandalizi Kizimkazi vilivyotolewa na NBC ikiwa ni sehemu ya shughuli za kuisaidia jamii za benki hiyo zinazoendelea kufanyika sehemu mbalimbali nchini. Makabidhiano hayo yalifanyika shuleni hapo Visiwani Zanzibar jana.
Meneja wa Tawi la Benki ya NBC Zanzibar, Ramadhani Lesso (katikati, mwenye suti nyeusi) akikabidhi baadhi ya vifaa vya ujenzi vikiwemo mabati  140 pamoja na vifaa vingine vya kuezekea vyenye thamani zaidi ya shilingi  milioni 8 kwa baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Maandalizi ya Kisimkazi vilivyotolewa na NBC mjini Zanzibar jana. Wa nne kushoto ni Mkuu wa Mkoa Kusini Unguja, Hassan Khatibu Hassan.
Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja, Hassan Khatibu Hassan (wa pili kushoto), akizungumza kabla hajapokea msaada wa mabati  140 pamoja na vifaa vingine vya kuezekea vyenye thamani  ya zaidi ya shilingi  milioni 8 kutoka benki ya NBC kwa ajili ya kuezekea madarasa manne pamoja na ofisi mbili za walimu za shule ya Maandalizi Kizimkazi katika hafla iliyofanyika visiwani Zanzibar jana. Wa nne kulia ni Meneja wa NBC Zanzibar, Ramadhani Lesso.
Meneja wa Tawi la Benki ya NBC Zanzibar, Ramadhani Lesso (wa pili kulia) akizungumza katika hafla ya kukabidhi msaada wa mabati  140 pamoja na vifaa vingine vya kuezekea vyenye thamani  ya zaidi ya shilingi  milioni 8 kwa ajili ya kuezekea madarasa manne pamoja na ofisi mbili za walimu za shule ya Maandalizi Kizimkazi vilivyotolewa na benki hiyo visiwani Zanzibar jana. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja, Hassan Khatibu Hassan.

Comments are closed.