The House of Favourite Newspapers
gunners X

Nchi 13 Ambazo Hazijapata Maambukizi ya Corona

0

MPAKA kufikia Desemba mwaka 2019 homa ya kirusi cha corona ilikuwa nchini China tu. Lakini majuma machache baadaye ikaanza kusambaa maeneo mbalimbali duniani na kugeuka kuwa janga la afya la kiulimwengu.

 

Kirusi huyo ambaye huathiri mfumo wa upumuaji wa binadamu hivi sasa tayari kimeripotiwa kuwepo katika nchi 185.

 

Wanasayansi duniani kote wanasisitiza watu kuchukua hatua za tahadhari kujilinda na maambukizi ikiwemo kuepuka mikusanyiko.  Kwa mujibu wa takwimu za Chuo Kikuu cha Johns Hopkins nchini Marekani, zaidi ya watu milioni tatu wameambukizwa ugonjwa huo. 

Hapa nchini ni nchi chache ambazo hadi kufikia asubuhi ya leo Mei 4 saa za Afrika Mashariki hazijaripoti kuwa na mgonjwa hata mmoja wa homa ya kirusi cha corona (COVID-19).

 

Kiribati (Kisiwa)

Lesotho

Visiwa vya Marshall

Micronesia (Kisiwa)

Nauru (Kisiwa) 

North Korea

Palau (Kisiwa)

Samoa (Kisiwa)

Visiwa vya Solomon 

Tonga (Kisiwa)

Turkmenistan

Tuvalu (Kisiwa)

Vanuatu (Kisiwa).

Leave A Reply