The House of Favourite Newspapers

Nchi 33 Zinatarajia Kushiriki Mkutano 13 wa Taasisi za  Jumuiya ya Skauti Wakike  Bara la  Afrika

0
AKRIBANI nchi 33 zinatarajia kushiriki mkutano 13 wa Taasisi za  Jumuiya ya Skauti wakike  bara la  Afrika (Taasisi ya Girl Guide)  nchini Tanzania na  kuwakutanisha wajumbe  kutoka nchi hizo ambao ni wanachama  wa World Association of Girl Guides and Girl Scous (WAGGGS).
Nchi hizo zinakutana kwa lengo la kutathmini hatua walizopiga kwa miaka mitatu iliyopita,tathmini ya Changamoto na mafunzo  yaliyotokana na janga la Uviko 19,Kuweka mikakati mipya na kuchagua Uongozi wa kipindi kingine cha miaka mitatu kuanzia sasa.
Hayo yamesemwa jana  jijini Dar es Salaam na Kamishna  Mkuu wa Jumuiya ya Skauti wakike Tanzania,Wakili  Mary Richard alisema  mkutano huo kufanyika nchini ni nafasi ya kuona na kujifunza kutoka  kwa nchi zingine  namna ambavyo wanaendesha shughuli zao za guiding.
Alisema mkutano huo pia  utakuwa ni sehemu ya kukuza ufanisi na utendaji wa Chama kwani utaleta kundi la watu  zaidi ya 120 nchini.
“Katika Mkutano huub,kutakuwa na hafla za ufunguzi  kufunga na usiku wa Utamaduni ambapo inatarajiwa kufanyika Agosti 22 hadi 26,mwaka huu katika ukumbi wa  Julius Nyerere International Convention  Centre,”
alisema na kuongeza
Leave A Reply