NDALICHAKO, MASAUNI WATOA POLE KWA FAMILIA YA AKWILINA
Waziri wa Elimu Pro. Joyce Ndalichako na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni, jioni ya leo wamefika nyumbani kwa marehemu Akwilina Akwiline huko Mbezi, jijini Dar es Salaam, kuwafariji wanafamilia.
Wakati huohuo, Rais John Magufuli ametoa pole kwa wanafamilia hao na ameagiza hatua kali na za haraka kuchukuliwa dhidi ya waliohusika kumpiga risasi marehemu Akwilina.
Comments are closed.