The House of Favourite Newspapers

NDALICHAKO, MASAUNI WATOA POLE KWA FAMILIA YA AKWILINA

Waziri wa Elimu Profesa. Joyce Ndalichako (katikati) akiwa katika msiba huko Mbezi, Dar es Salaam, na mmoja wa mama  wa marehemu aliyekuwa  mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini ambaye aliuawa kwa kupigwa risasi Ijumaa wiki hii eneo la Mkwajuni, Kinondoni, Dar.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,  Hamad Masauni (kulia mwenye suti nyeusi) akitoa pole wafiwa.
…Akiongea jambo katika msiba huo.

Waziri wa Elimu Pro. Joyce Ndalichako  na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni, jioni  ya leo wamefika nyumbani kwa marehemu Akwilina Akwiline huko Mbezi, jijini Dar es Salaam, kuwafariji wanafamilia.

Wakati huohuo, Rais John Magufuli ametoa pole kwa wanafamilia hao na  ameagiza hatua kali na za haraka kuchukuliwa dhidi ya waliohusika kumpiga risasi marehemu Akwilina.

Comments are closed.