NESI mmoja nchini Malawi amesimamishwa kazi baada ya ‘selfie’ aliyojipiga katika wodi ya wajawazito kumwonyesha nyuma yake mwanamke mmoja mjamzito aliyekuwa mtupu (hana nguo). Selfie hiyo ya Patricia Malichi inayomwonyesha mwanamke asiyefahamika akiwa amelala kitandani katika Kituo cha Afya cha Ndirande jijini Blantayre, ilizua chuki katika mitandao ya kijamii ambapo Wamalawi wengi walitaka afukuzwe kazi.
Comments are closed.