The House of Favourite Newspapers

Ngariba wa Wakurya Dar Aibuka, Awatahiri Watoto Saa 9 Usiku!

ngariba-wa-kikurya-3 Na Gabriel Ng’osha | Gazeti la Uwazi, Toleo la Desemba 20, 2016

TOHARA ni jambo la muhimu na la lazima miongoni mwa vijana wa Kabila la Wakurya, linalopatikana Mkoa wa Mara. Jambo hili la kimila, kwa kawaida hufanyika Desemba ya kila mwaka, ambapo vijana wa kike na kiume hufanyiwa tendo hilo linalotafsiriwa kama kukua kwao.

Kwa kawaida tohara hufanywa na watu maalum, waitwao mangariba, ambao wazazi hulazimika kuwapeleka watoto wao kwa wataalam hao ambao hutumia vifaa vya kijadi huku zoezi lenyewe, likifanyika usiku.

Kutokana na kusambaa kwa watu wa kabila hilo katika mikoa mbalimbali na ugumu wa maisha pamoja na umbali uliopo, baadhi wameshindwa kurejea nyumbani kufanya zoezi hilo, badala yake wameamua kufanyia huko wanakoishi.

ngariba-wa-kikurya-2Wakurya wakisherehekea vijana kufanyiwa tohara.

Jijini Dar es Salaam, ambako jamii kubwa ya kabila hilo wanaishi maeneo ya Kivule na Kitunda, nao wameamua kufanyia tohara huko wanakoishi, lakini wakienda sawa na wenzao waliopo nyumbani mkoani Mara.

Baada ya zoezi hilo kufanyika usiku wa manane, mapema asubuhi hufuatiwa na sherehe kubwa ya kushangiliwa kwa kufanikishwa kwa zoezi hilo, linaloenda sambamba na washangiliaji kubeba silaha za jadi kama mapanga, visu, sime na mikuki.

Leo, mwandishi wetu anakutana na Ngariba, mzee Mwita Matiku ‘Mwita Dokta’ (52), ambaye anafunguka kuhusu suala zima la tohara kwa jamii yake.

ngariba-wa-kikurya-5Ngariba, mzee Mwita Matiku ‘Mwita Dokta’ akizungumza na mwanahabari wetu (hayupo pichani)

“Suala la kutahiriwa kwa vijana kuanzia miaka 14 na kuendelea kwa jamii ya Wakurya ni la kawaida sana na hata utaratibu wa kushangilia baada ya kuwatahiri watoto wetu umekuwepo kwa miaka mingi sana.

ngariba-wa-kikurya-1“Kwa sisi ambao tuko Dar es Salaam, hatuwezi kufunga safari ya kwenda Mkoa wa Mara kila mwaka kwa ajili ya kwenda kuwatahiri watoto wetu, hivyo tumekuwa tukisubiri wazee wa kimila kule Mara wakianza zoezi hilo basi na sisi tulioko Dar tunaanza.

“Ni kama sherehe ya kimila ndiyo maana wakimaliza kutahiriwa, wazazi wa wahusika huamua kufanya sherehe kwa kuchinja mbuzi au ng’ombe kisha kuwaalika jamaa zao.

ngariba-wa-kikurya-6“Mara nyingi hutahiriwa majira ya kuanzia saa 9 hadi 11 alfajiri kwa sababu damu inakuwa baridi hivyo haiwezi kuvuja nyingi.

“Nimekuwa nikiwatahiri vijana wengi sana kwa miaka sita sasa na mwaka jana nilitahiri vijana zaidi ya 200 ila mwaka huu nimewahudumia vijana 50 kwa sababu kuna ngariba mwingine ameibuka maeneo haya.

“Wanapotoka kutahiriwa majira ya alfajiri ndipo hupokelewa na ndugu zao kishujaa wakiwa na mapanga, mishale, mikuki, fimbo huku wengine wakiwa wamejipaka damu, wamevaa majani na kadhalika. Hupita mitaani huku wakishangilia kama alama ya watoto wao kukua na kuitwa wanaume kamili.

ngariba-wa-kikurya-7“Tohara yangu mimi ni ya kitaalamu na nina taaluma ya uuguzi, kwani ninafanya vitu vyote ambavyo hufanywa hospitalini ikiwemo kusafisha vifaa vya kukatia, kufunga kidonda, kushona, kusafisha kwa kuchemsha vifaa pamoja na kutumia kifaa kipya kwa kila mtahiriwa.

“Mara nyingi gharama ya kutahiriwa huwa ni maelewano lakini huanzia shilingi 30,000 kwa kijana mmoja. Mwaka huu kwangu itakuwa ni wa mwisho, inabidi niwapishe na vijana wafanye kazi hiyo.

ngariba-wa-kikurya-4“Kwangu mimi sijawahi kufanya tohara kwa watoto wa kike, kwanza siruhusiwi kutokana na jinsia yangu na kama wanafanya basi itakuwa ni usiku na kwa kificho sana maana serikali imepiga marufuku kitu hicho hata jamii yetu nayo inazidi kuelimika juu ya madhara ya tohara kwa wanawake,” anasema mzee Mwita.

Irene Uwoya Afanya Kufuru Birthday Yake, Amkumbuka Samwel Sitta Aliyezaliwa Naye Des. 29

Comments are closed.