The House of Favourite Newspapers

Nikki wa Pili: Mashabiki Wamekacha Shoo!

nikki-wa-pili

Nikki wa Pili

GAZETI LA IJUMAA JANUARI 20 RAPA anayefanya poa katika Muziki wa Hip Hop Bongo, Nickson Simon ‘Nikki wa Pili’ amekiri mashabiki wengi kuacha kujitokeza katika shoo mbalimbali nchini kutokana na uchumi kuyumba.

Akizungumza na Showbiz, Nikki wa Pili anayebamba na Ngoma ya Sweet Mangi alisema, amekuwa akisikia kuyumba kwa uchumi na wasanii wengi wa Bongo Fleva wamekuwa wakitegemea kupata hela kupitia shoo lakini kwa hali ya sasa ilivyo imekuwa ngumu.

nikki-wa-pili

Nikki wa Pili

“Kwa sasa huwezi kukuta mashabiki wanajitokeza kwa wingi kwenye burudani kama zamani kwa sababu mfukoni hawana kitu. Mashabiki wengi bajeti zao wamezielekeza kwenye mahitaji muhimu tu, burudani wameiweka kando kwa muda, maana yake ni kwamba kazi ya muziki tunapolekea itakuwa mbaya,” alisema Nikki.

Comments are closed.