The House of Favourite Newspapers

Nilifanya Map enzi na Maiti 20 Ili Nitajirike- 21

0

ILIPOISHIA

…ile maiti ikainuka kisha kukaa kitako mle kwenye sanduku. Mpaka kufikia hatua hiyo, nilitamani kukimbia. Jasho lilinitoka.

SONGA NAYO
Kuna kipindi nilihisi kile kilichokuwa kikitokea kilikuwa ni ndoto, nilitamani kukimbia lakini miguu ilikuwa mizito.

Kadiri muda ulivyozidi kusonga mbele ndivyo nilivyozidi kushikwa na hofu. Kumbuka kwamba hiyo ilikuwa usiku wa manane, tena tukiwa mochwari, najua umeshapata picha ni jinsi gani nilikuwa na hofu moyoni mwangu.

Yule mganga hakunyamaza, akawa anazungumza maneno ambayo sikuyaelewa kabisa. Aliponitupia macho niliyahamisha yangu na kuiangalia ile maiti iliyokuwa imeketi kitako kama mtu aliyekuwa akitaka kuzungumza na yule mganga.

“Usiogope Zakia,” aliniambia huku akiniangalia lakini nilikuwa na hofu.
Nikaanza kuyakumbuka maneno ya yule mganga aliyoniambia kipindi cha nyuma kwamba kama kweli nilitaka kuwa tajiri basi ilinibidi nikubali sharti la kufanya mapenzi na maiti ishirini, kwa hiyo ile maiti iliyokuwa mbele yangu ilikuwa ya kwanza.

Nilikubali lakini ndani ya mochwari ile lilionekana kuwa jambo gumu mno, kufanya mapenzi na maiti. Tena kama ile iliyokuwa ikitisha iliyoonekana kabla ya kuwa maiti, mtu huyo alipata ajali mbaya, kama si gari, basi ilikuwa treni kwani mwili wake ulikuwa na majeraha mengi.
“Njoo huku,” aliniambia yule mganga, nikaanza kusogea kule alipokuwa.
Akaniambia nikae kwanza, nilitakiwa kuvuta pumzi na sikutakiwa kuogopa. Nilikuwa kimya, nilikuwa na hofu sana nikiogopa.

Maiti ile ikafumbua macho yake na kuanza kuniangalia, kuna kipindi nilikuwa nikijiuliza kama kweli ile ilikuwa maiti au nilikuwa nikichezewa mchezo. Majibu ya Swali langu hilo lilipatikana kila nilipokuwa nikiuangalia mwili wake, ilionesha dhahiri kwamba ilikuwa maiti.
“Upo tayari?” aliniuliza mganga.
“Ndiyo! Ila….”
“Ila nini tena?”
“Nitaweza kweli?”

“Usijali! Utaweza. Kwani hujawahi kufanya mapenzi na mwanaume?” aliuliza mganga huku akiniangalia usoni.
“Nimewahi!”
“Basi jua hakuna tatizo,” aliniambia.
Nilibaki nikimwangalia tu, kuna kipindi nilijuta kwa nini nilitaka kuwa tajiri na wakati masharti ya utajiri wenyewe yalikuwa magumu kiasi hiki. Nilibaki nikisononeka lakini kumbuka kwamba nilitamani kuwa tajiri hivyo chochote kilichokuwa kinatokea mbele yangu, nilikubaliana nacho.
“Vua nguo zako,” aliniambia.

Wakati hayo yakiendelea ndani ya mochwari, wale walinzi hawakuwa wakijua kitu chochote kile, hawakutuona hivyo kufanya kila kitu kwa kujiachia. Baada ya kumaliza kuvua nguo zangu na kubaki kama nilivyozaliwa, akaniambia nipande juu ya meza, nikafanya hivyo, nikalala chali.
Ndugu yangu, ninachokwambia hapa ni kweli kabisa, kilinitokea katika maisha yangu, kipindi kile nilipokuwa nikisaka utajiri kwa udi na uvumba. Ghafla nikaiona maiti ile ikisimama kutoka ndani ya sanduku na kuanza kuvua nguo zake zilizokuwa zimechanikachanika kutokana na ajali, baada ya hapo, akapanda pale juu.

“Mkimaliza, utatoka nje, hili sanduku usiwe na hofu nalo, litarudi tu lilipokuwa,’ aliniambia yule mganga.

yule na kisha yeye kutoka ndani ya mochari ile na kwenda kunisubiri nje.
Kilichoendelea ndani, ni kufanya mapenzi na maiti ile. Huwa ninasikia maumivu mno moyoni mwangu kila ninapokumbuka mambo haya ambayo yalinitokea. Ninaamini kwamba mtu anapokufa, kuna roho huwa inabaki na ndiyo maana unapofika makaburini usiku, kuna sauti huwa zinasikika, mbali na roho iliyokufa, kunakuwa na roho nyingine ambayo bado ina uhai.

Hiyo ndiyo roho aliyokuwa nayo ile maiti, roho yake ya kwanza ilikuwa imekwishatoka na kwenda kwenye hukumu, iliyokuwa ikifanya yote hayo ni roho ya pili ambayo ilimpa pumzi.
Pale juu, niliendelea kufanya mapenzi na maiti ile, ilikuwa ni kama nafanya mapenzi na binadamu aliyekuwa hai. Nilisikia maumivu makali chini ya kitovu, nilipiga kelele lakini haikujali, iliendelea kama kawaida yangu.

Kitendo kile kilichukua dakika arobaini, ilipomaliza, ikasimama, ikavaa na kisha kuingia ndani ya sanduku lile. Sikuvaa, nilibaki kuangalia nione kitu gani kingetokea. Wakati imeingia kwenye sanduku lake, likajifunga na kuanza kuinuka, likajiingiza katika sehemu yake na kutulia.

Sikutaka kubaki humo, nilichokifanya ni kuinuka, kuvaa nguo zangu na kutoka ndani ya mochwari ile. Walinzi walikuwa wakipiga stori, sikujali, nikatoka mpaka nje, nilipofika huko, nikamkuta mganga akiwa na tabasamu pana kabisa huku akitingisha kichwa chake juu chini, chini juu kuonyesha kukubaliana na kile kilichofanyika.
Itaendelea wiki ijayo.

Leave A Reply