The House of Favourite Newspapers

Nilifanya Mapenzi na Maiti 20 Nitajirike – 11

maiti-cover

ILIPOISHIA SEHEMU YA 10

YULE mzee sikuweza kumfahamu kwa kipindi kile lakini sauti yake, hapo baadaye nilimfahamu kwani nilikutana naye mara kwa mara. Baada ya kuzungumza hivyo, akatoa kidumu na kumpa mlinzi yule ambaye akakichukua na kuondoka nacho.

Sikutaka kubaki hapo nje, nikamfuata mlinzi mule mochwari alipokwenda. Nilipoingia, nikakuta akimwambia mwenzake kwamba kulikuwa na dili jingine, kuna mtu alifuata maji ya maiti.

“Hakuna tatizo! Twende kule kwenye maiti za wiki iliyopita!” alisema mlinzi aliyeletewa taarifa.

MWAGIKA NAYO HAPA…

Wakatoka na kuelekea kwenye moja ya masanduku yaliyokuwa mwisho kabisa ambayo yalikuwa na maiti zilizokuwa na muda mrefu humo mochwari. Wakafungua sanduku moja, wakatoa maiti ya msichana na kuiweka juu ya meza moja kisha kuanza kuiosha huku wakikinga maji na kuyaweka katika sufuria kubwa kabla ya kuyaweka katika kidumu kile.

“Mungu! Kumbe haya ndiyo yanayotokea!” nilijikuta nikisema.

Waliendelea na zoezi lao mpaka walipomaliza na kujaza kile kidumu, yule mlinzi akaelekea nje na kumpa yule mzee, gari likawashwa na kuondoka mahali hapo.

Wakati ikiwa imefika saa nane usiku, hapo ndipo mganga yule akatokea hapo ndani na kunifuata. Kabla ya kuzungumza lolote, akaniangalia machoni, aliiona hofu niliyokuwa nayo.

“Upo sawa?” aliniuliza.

“Ndiyo! Nipo sawa na nipo tayari kwa kazi,” nilimwambia.

Alichokifanya mganga yule ni kuuchukua usinga wake, akaanza kuimba wimbo ambao sikuwa nikiuelewa. Aliimba kwa sauti kubwa iliyonifanya nione kama wale walinzi wangesikia lakini haikuwa hivyo.

Waliendelea kupiga stori huku mganga yule akiendelea na wimbo wake. Alipomaliza, akalifuata sanduku moja, akalitoa pale lilipokuwa. Nilibaki nikiwa nimeduwaa tu, sikuamini kilichokuwa kikiendelea, sanduku lilikuwa zito lakini yeye alivyolishika ilikuwa ni kama mtu aliyeshika kikaratasi.

Akaliweka chini, akalifungua na kisha kuiangalia maiti ile. Niliogopa, hata kusogea kule sikuweza. Wakati nimesimama huku nikiwa nimeduwaa, yule mganga akachukua unga fulani na kuipaka maiti ile kisha kuanza kuzungumza maneno ambayo sikuyaelewa, ghafla, katika hali iliyonishtua, nikaiona maiti ile ikiinua mkono wake.

“Mungu wangu!” nilisema kwa mshtuko, sikuamini kile nilichokiona. Mganga yule hakunyamaza, aliendelea kuzungumza maneno yale, mbali na mkono, ile maiti ikainuka na kisha kukaa kitako mulemule kwenye sanduku. Mpaka kufikia hatua hiyo, nilitamani kukimbia. Jasho lilinitoka.

Kuna kipindi nilihisi kile kilichokuwa kikitokea kilikuwa ni ndoto, nilitamani kukimbia lakini miguu ilikuwa mizito.

Kadiri muda ulivyozidi kusonga mbele ndivyo nilivyozidi kushikwa na hofu. Kumbuka kwamba hiyo ilikuwa usiku wa manane, tena tukiwa mochwari, najua umeshapata picha ni jinsi gani nilikuwa na hofu moyoni mwangu.

Yule mganga hakunyamaza, akawa anazungumza maneno ambayo sikuyaelewa kabisa. Aliponitupia macho niliyahamisha yangu na kuiangalia ile maiti iliyokuwa imeketi kitako kama mtu aliyekuwa akitaka kuzungumza na yule mganga.

“Usiogope Zakia,” aliniambia huku akiniangalia lakini nilikuwa na hofu.

Nikaanza kuyakumbuka maneno ya yule mganga aliyoniambia kipindi cha nyuma kwamba kama kweli nilitaka kuwa tajiri basi ilinibidi nikubali sharti la kufanya mapenzi na maiti ishirini, kwa hiyo ile maiti iliyokuwa mbele yangu ilikuwa ya kwanza.

Nilikubali lakini ndani ya mochwari ile lilionekana kuwa jambo gumu mno, kufanya mapenzi na maiti. Tena kama ile iliyokuwa ikitisha iliyoonekana kabla ya kuwa maiti, mtu huyo alipata ajali mbaya, kama si gari, basi ilikuwa treni kwani mwili wake ulikuwa na majeraha mengi.

“Njoo huku,” aliniambia yule mganga, nikaanza kusogea kule alipokuwa.

Akaniambia nikae kwanza, nilitakiwa kuvuta pumzi na sikutakiwa kuogopa. Nilikuwa kimya, nilikuwa na hofu sana nikiogopa.

Maiti ile ikafumbua macho yake na kuanza kuniangalia, kuna kipindi nilikuwa nikijiuliza kama kweli ile ilikuwa maiti au nilikuwa nikichezewa mchezo. Majibu ya Swali langu hilo lilipatikana kila nilipokuwa nikiuangalia mwili wake, ilionesha dhahiri kwamba ilikuwa maiti.

“Upo tayari?” aliniuliza mganga.

“Ndiyo! Ila….”

“Ila nini tena?”

“Nitaweza kweli?”

“Usijali! Utaweza. Kwani hujawahi kufanya mapenzi na mwanaume?” aliuliza mganga huku akiniangalia usoni.

“Nimewahi!”

“Basi jua hakuna tatizo,” aliniambia.

Nilibaki nikimwangalia tu, kuna kipindi nilijuta kwa nini nilitaka kuwa tajiri na wakati masharti ya utajiri wenyewe yalikuwa magumu kiasi hiki. Nilibaki nikisononeka lakini kumbuka kwamba nilitamani kuwa tajiri hivyo chochote kilichokuwa kinatokea mbele yangu, nilikubaliana nacho.

“Vua nguo zako,” aliniambia.

Wakati hayo yakiendelea ndani ya mochwari, wale walinzi hawakuwa wakijua kitu chochote kile, hawakutuona hivyo kufanya kila kitu kwa kujiachia. Baada ya kumaliza kuvua nguo zangu na kubaki kama nilivyozaliwa, akaniambia nipande juu ya meza, nikafanya hivyo, nikalala chali.

Ndugu yangu, ninachokwambia hapa ni kweli kabisa, kilinitokea katika maisha yangu, kipindi kile nilipokuwa nikisaka utajiri kwa udi na uvumba. Ghafla nikaiona maiti ile ikisimama kutoka ndani ya sanduku na kuanza kuvua nguo zake zilizokuwa zimechanikachanika kutokana na ajali, baada ya hapo, akapanda pale juu.

“Mkimaliza, utatoka nje, hili sanduku usiwe na hofu nalo, litarudi tu lilipokuwa,” aliniambia yule mganga na kisha yeye kutoka ndani ya mochwari ile na kwenda kunisubiri nje.

****

Je, nini kitaendelea? Usikose kufuatilia kesho hapa kujua kitakachoendelea katika sehemu ya 12

MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI

Video: Alichokizungumza Mzee wa Miaka 76 Aliyeweka Bango Kutafuta Mwanamke wa Kuoa

halotel-strip-1-1

Comments are closed.