Nilifanya Mapenzi na Maiti 20 Nitajirike – 12
ILIPOISHIA
“Mkimaliza, utatoka nje, hili sanduku usiwe na hofu nalo, litarudi tu lilipokuwa,’ aliniambia yule mganga.
yule na kisha yeye kutoka ndani ya mochari ile na kwenda kunisubiri nje.
ENDELEA NAYO
Kilichoendelea ndani, ni kufanya mapenzi na maiti ile. Huwa ninasikia maumivu mno moyoni mwangu kila ninapokumbuka mambo haya ambayo yalinitokea. Ninaamini kwamba mtu anapokufa, kuna roho huwa inabaki na ndiyo maana unapofika makaburini usiku, kuna sauti huwa zinasikika, mbali na roho iliyokufa, kunakuwa na roho nyingine ambayo bado ina uhai.
Hiyo ndiyo roho aliyokuwa nayo ile maiti, roho yake ya kwanza ilikuwa imekwishatoka na kwenda kwenye hukumu, iliyokuwa ikifanya yote hayo ni roho ya pili ambayo ilimpa pumzi.
Pale juu, niliendelea kufanya mapenzi na maiti ile, ilikuwa ni kama nafanya mapenzi na binadamu aliyekuwa hai. Nilisikia maumivu makali chini ya kitovu, nilipiga kelele lakini haikujali, iliendelea kama kawaida yangu.
Kitendo kile kilichukua dakika arobaini, ilipomaliza, ikasimama, ikavaa na kisha kuingia ndani ya sanduku lile. Sikuvaa, nilibaki kuangalia nione kitu gani kingetokea. Wakati imeingia kwenye sanduku lake, likajifunga na kuanza kuinuka, likajiingiza katika sehemu yake na kutulia.
Sikutaka kubaki humo, nilichokifanya ni kuinuka, kuvaa nguo zangu na kutoka ndani ya mochwari ile. Walinzi walikuwa wakipiga stori, sikujali, nikatoka mpaka nje, nilipofika huko, nikamkuta mganga akiwa na tabasamu pana kabisa huku akitingisha kichwa chake juu chini, chini juu kuonyesha kukubaliana na kile kilichofanyika.
****
Mganga alinipa uhakika kwamba kila kitu kingekuwa kama kilivyotakiwa kuwa. Kwa kweli nilimwamini sana na kuona kuwa hivi karibuni ningekuwa tajiri mkubwa mno nchini Tanzania na hivyo kurudi kijijini nikiwa shujaa.
Siku iliyofuata, mganga akaniambia nirudi nilipokuwa nikiishi ambapo sikutakiwa kumwambia mtu yeyote juu ya kile kilichokuwa kimetokea. Sasa ratiba ikawa ni kwenda kwa mganga kila siku, ananichukua kimazingara na kunipeleka mochwari ambapo kama kawaida nilikuwa nikiendelea kufanya mapenzi na maiti.
Siku ya kwanza niliogopa sana lakini siku zilivyoendelea kwenda, hofu ikaniondoka na hivyo kuwa na ushujaa mkubwa moyoni mwangu. Nilipitia mengi kipindi hicho, wakati mwingine nililetewa maiti zilizoungua moto, zilitisha sana lakini ilikuwa ni lazima nifanye nazo mapenzi, wakati mwingine nililetewa maiti zilizopata majanga mengine, zote hizo, nilivumilia.
Siku zilikatika mpaka nilipobakiza maiti moja. Mganga akaniambia kwamba hiyo sikutakiwa kufanya nayo kule mochwari bali nilitakiwa kufanya nayo sehemu nyingine kabisa, tena makaburini.
Kwa kweli niliogopa sana, sikujua kitu kilichonitisha kwani kiukweli kati ya makaburini na mochwari, mochwari kulitisha zaidi. Usiku, mganga akanichukua na kuniepeleka katika makaburi fulani yaliyokuwa jijini Dar. Nilipofika karibu na makaburi hayo, akaniambia niingie ndani ya eneo la makaburi na kisha kuelekea katika kaburi moja la jamaa mmoja aliyekufa miaka kumi iliyopita, huyo jamaa aliitwa Samweli Ramadhani.
“Nitalijuaje?”
“Utalijua tu, una uwezo mkubwa wa kulijua kaburi hilo, wewe nenda,” aliniambia mganga.
Wakati nimeingia ndani ya eneo la kaburi hilo, kwa macho yangu niliweza kuwaona wachawi, walikuwa zaidi ya ishirini, walisimama pembeni ya kaburi moja la mtoto ambapo maiti yake ilikuwa ikihitajika sana.
Sikujua kwa nini, sikufika pale kuwafuatilia achawi wale niliowaona ila wao hawakuniona, nilifika pale nikiwa na mambo yangu, hivyo sikujali. Nilitembea kwa tahadhari, makaburini kulitisha sana, kulisisimua kupita maelezo.
Nilipofika katika kaburi moja, nikasimama, sikujua kama lilikuwa lenyewe au jingine, nikasogelea kuangalia jina, nikakuta limeandikwa Samweli Ramadhani, nikashangaa, nimejuaje kama hilo kaburi ndilo lenyewe.
“Ila kwa nini maiti hii?” nilijiuliza, ghafla nikasikia mganga akinijibu.
“Kwa imani zetu wanadamu, tunasema jina la Samweli ni la Kikristo na Ramadhani ni la Kiislamu, hivyo ukifanya mapenzi na maiti hii, Wakristo na Waislamu wote watakuheshimu, na utajiri wako utamsisimua kila mtu,” nilimsikia vema mganga huyo.
Nilisimama huku nikiwa sijui nini cha kufanya, nilisubiri maelekezo, nikaisikia sauti ya mganga ikiniambia nisubiri, nikafanya hivyo, ghafla, katika hali ambayo sikuitarajia, nikaona hirizi kubwa ikiwa imefungwa kiunoni mwangu, ilikuwa nzito, kilichonishangaza, hirizi ile kama ilikuwa na moyo, kwani niliweza kuyasikia mapigo kama ya moyo yakidunda kutoka katika hirizi hiyo.
Mara ghafla, upepo mkali ukaanza kuvuma mahali hapo, matawi ya miti iliyokuwa makaburini hapo yakaanza kuyumbishwa huku na kule. Nikasikia kelele za watu wengi, sikujua zilitoka wapi lakini nilizisikia masikioni mwangu.
Nikaanza kutetemeka, mara nikahisi kama kuna mtu alikuwa nyuma yangu, sikugeuka kuona alikuwa nani, mtu huyo akanisogelea, na kunishika bega kwa nyuma, pumzi zake nilisikia vema karibu kabisa na masikio yangu . Nikashindwa kuvumilia, nikageuka nyuma, cha kushangaza sikuona mtu.
Wakati nikiendelea kutetemeka kaburini pale, ghafla nikaliona lile kaburi likianza kujifukua lenyewe na ndani yake kuona jeneza likiwa limefunguliwa na ndani yake hakukuwa na maiti yoyote ile, nikashangaa sana.
Mara ghafla mwili wangu ukaanza kusisimka sana, nikahisi tena kwamba nyuma yangu kulikuwa na mtu, nilitaka kugeuka, nikashindwa kufanya hivyo, nikahisi nikishikwa bega kwa nyuma, nilitetemeka zaidi, kijasho chembamba kikanitoka mno.
“Unanukia vizuri mpenzi wangu!” nilisikia sauti hiyo nyuma yangu, nikazidi kutetemeka.
“Wewe nani?” nilijikuta nikiuliza huku mihemo ya mtu huyo ikisikika vema nyuma yangu.
Niliuliza swali hilo huku nikitetemeka sana, nilitamani nipotee na kutokea sehemu tofauti na hiyo. Mwili haukuacha kusisimka, kuna kipindi niliyasikia kabisa mapigo yangu ya moyo yalivyokuwa yakidunda kwa nguvu.
“Mimi ni mpenzi wako uliyemfuata hapa makaburini, una ngozi laini sana, hakika wewe ni mwanamke wa ndoto yangu,” niliendelea kuisikia sauti hiyo.
Mara mguso wa mtu huyo ukahama kutoka begani mwangu na kuanza kuelekea chini, nilizidi kutetemeka mno, mikono yake ikahamia katika mgongo wangu na kuanza kuushikashika, baadaye akahamia katika kiuno changu, nikabaki nikianza kulegea mwili wangu.
“Ni kipindi kirefu kimepita, miaka kumi pasipo kumgusa mwanamke yeyote yule, upo tayari mpenzi wangu?” aliniuliza.
Sikumjibu, nilibaki kimya, wakati nikiwa nimesimama vilevile, ghafla nikaanza kuona mazingira ya mahali pale yakianza kuondoka na mazingira mengine kuingia.
Mbele yangu kukaonekana kuwa na kitanda kikubwa, ndani ya chumba kikubwa, alichonifanya ni kunisukumia kitandani, niliona kweli nimeangukia kitandani, ila ukweli ni kwamba niliangukia ndani ya kaburi lake, kitanda, lilikuwa jeneza lake, alichokifanya, naye akaja kwa juu yangu mgongoni, nikajigeuza ili nimuone, sikumuona, ila miguso yake, ilionyesha kabisa kwamba alikuwa hapo pamoja nami kwani yeye ndiye alianza kunivua nguo, yaani nalivuliwa nguo na mtu nisiyemuona.
Nilitakiwa kutulia vilevile, kumbuka kwamba nilifanya mapenzi na maiti kumi na tisa na hiyo ndiyo ilikuwa ya mwisho, hivyo niliona kuwa na sababu zote za kutulia kwani baada ya hapo, nilikuwa na uhakika wa kupata utajiri kama alivyoniambia mganga yule.
Ndani ya kaburi lile ndipo tulipoanza kufanya mapenzi, maiti ile ilikuwa ikinuka sana, sikuwa nikiiona ila niliihisi miguso yake kila kona katika mwili wangu.
Nilifanya naye mapenzi kwa saa moja ndipo akamaliza, nikahisi akiondoka mahali hapo na kuisikia sauti ya mganga ikinipongeza kwa kazi nzuri niliyoifanya, sasa ningekuwa tajiri mkubwa.
“Umefanikiwa, sasa utakuwa tajiri mkubwa tu,” nilisikia sauti ya mganga.
Nilichokifanya ni kutoka nje ya kaburi na kuvaa nguo zangu. Kilichonishangaza, ghafla nikaanza kuona moshi mzito ukifuka kutoka ndani ya kaburi lile, sikujua nini kiliendelea, moshi ule mzito ukalifunika kaburi lote hata lisionekane, wakati nashangaashangaa tu, ghafla moshi ule ukakatika na kaburi lile kujifukia kama lilivyokuwa mwanzo.
Sikutaka kubaki mahali hapo, nikatoka na kuelekea nje ya eneo la kaburi lile huku tayari ikiwa ni saa nane usiku. Nilimkuta mganga akiwa amekaa pembeni akinisubiri, aliponiona, kwanza akatoa tabasamu pana, nikamsogelea.
“Hongera sana, hakika umenifanya nijisikie fahari sana,” aliniambia mganga yule.
“Kwa hiyo lini nitapata utajiri?”
“Utaanza kesho, ila nataka ufanye kitu.”
“Kitu gani?”
“Biashara yoyote ile…”
“Mmh!”
“Ndiyo hivyo! Utakapoanza, amini kwamba ndipo utajiri utakapoanzia..” aliniambia huku akinikazia macho.
Nilichokiamini ni kwamba mara baada ya kufanikiwa kufanya mapenzi na maiti zile basi ningepata utajiri kwa kukuta begi la fedha liwakiwa sehemu kumbe sivyo.
Akaniambia kwamba natakiwa kufanya biashara ambayo ndiyo ingekuwa chanzo cha utajiri wangu, sikuwa na jinsi, japo kwa kishingo upande, nikakubaliana naye. Na hivyo kuondoka mahali hapo.
Siku iliyofuata, nikamwambia Dickson pale Ubungo kwamba nilitaka kufanya biashara na biashara yenyewe ambayo niliichagua ilikuwa ni kuuza magazeti, akanikubalia hivyo kutafuta meza na kuanza kufanya harakati zote za kuhakikisha magazeti yanauzwa mara moja.
Siku mbili zilizofuata, tayari nilikuwa na meza yangu, niliweka juu magazeti mengi, nikatafuta vitabu vya hadithi na kutulia. Kitu cha ajabu ambacho sikuwahi kukiona ni pale watu walipoanza kumiminika katika meza yangu na kuanza kununua magazeti.
Nilishangaa, huwa ni vigumu kwa magazeti kumalizika kwa saa moja, lakini huwezi kuamini, magazeti mia moja niliyopewa, yote yaliishia ndani ya saa moja tu. Si mimi nileyeshangaa, hata watu wengine wa pale walishangaa pia.
Haikuwa kawaida kabisa na sidhani kama iliwahi kutokea. Magazeti yakaisha lakini nikashangaa watu wengine wakija mezani kwangu, waliiona meza ikiwa tupu ila wakawa wananiuliza kuhusu magazeti, yapo au yamekwisha, nilishangaa, meza ilikuwa tupu, sehemu zingine zilikuwa na magazeti, kwa nini hawakwenda huko?
Huo ulikuwa mwanzo, niliendelea kufanya biashara ya kuuza magazeti, ikaanza kuyabadilisha maisha yangu, nikawa naongezewa magazeti mengi, nikaanza kuyaona maisha yakianza kubadilika, fedha ziliingia, baadaye nikaanzisha biashara nyingine ya kuuza juisi na maji, hiyo ndiyo iliyoniingizia fedha zaidi na hivyo kupanga chumba Manzese Midizini.
Naweza kusema huo ulikuwa mwanzo tu, ndani ya miezi mitatu tangu nianze kufanya biashara hizo, nikashangaa nikiwa na akiba ya milioni tatu chumbani kwangu. Sikujua nilizipataje, ila nilichokijua ni kwamba kulikuwa na nguvu fulani nyuma yangu, nikafanikiwa zaidi.
Ulipoingia mwezi wa tano tangu nifanye biashara hizo, nikajikuta nikiwa na milioni tano. Nikashtuka, utajiri ukaanza kuninyemelea pasipo kukumbuka kwamba unapokuwa na utajiri wa kishetani huwa huna furaha, huna amani, ni utajiri unaotesa na kuumiza mno. Huo ndiyo ukaanza kuninyemelea. Mara ya kwanza, sikujali, ila baadaye, nilikuja kujuta kwa nini nilitaka utajiri.
Je, nini kitaendelea?
Comments are closed.