The House of Favourite Newspapers

Niliolewa na Mganga kwa tamaa ya cheo Kazini-22

0

ILIPOISHIA

Mmh, makubwa Rose alipofika mbele ya mzee Sionjwi alipiga magoti na kumpa maji kwa heshima zote. Mzee Sionjwi alichukua maji ya kunywa huku Rose akiwa bado amepiga magoti. 

Baada ya kunywa Rose alipokea kikombe huku mzee Sionjwi sijui nimwite dume la mbwa au jogoo la mtaa kila kuku jike wake, akisema.

SASA ENDELEA

“Asante mpenzi.”

“Asante kwa kushukuru mpenzi.”

Rose alinyanyuka na kuelekea ndani kurudisha kikombe, baada ya kunywa maji alimtuma bi mkubwa kwenda kumwekea maji ya kuoga. Aliniacha na baadhi ya wakeze na kwenda kuoga, Rose alirudi na kukaa huku akishika kiuno na kukunja uso.

“Vipi tena shoga?” nilimuuliza.

“Mmh, kiuno.”

“Kimefanya nini?”

”Toka jana na kila nikimweleza mzee Sionjwi anasema nisubiri zamu yangu ndiyo anipe tiba.”

“Kwani zamu yako lini?” Nilijitia umbea kuuliza yasiyonihusu.

“Leo usiku.”

“Sasa tiba mpaka ifike zamu yako?”

“Utamuweza mzee yule ngono itamuua anapenda kama chakula.”

Nilitamani kucheka kusikia hata wakeze wanajua kuwa bwana wao anapenda sana ngono.

“Si mtamuua ninyi wote wanne tena wote mpo kamili.”

“Kile kizee wanga tu hakina lolote.”

“Heheheheheheheeee….Rose utanivunja mbavu miye,” nilijikuta nacheka bila kupenda.

“Si utani Efrazia kama siyo wanga ni nini? Mtu kikongwe kama yule kuweza kugawa dozi kwetu sote tena si ya kitoto na bado yupo fiti.”

Nilijikuta nikiangua tena kicheko  mpaka machozi yakanitoka, niliamini ule ulikuwa muda muafaka wa kumuuliza ilikuwaje akaja kule kijijini na kuacha kazi ambayo ilimwongezea kipato ambacho kilisaidia familia yake.

“Rose mpenzi naomba nikuuliza kama nitakuudhi naomba unisamehe.”

“Mbona unanitisha ni swali gani hilo?”

“Ilikuwaje ukaja huku na kuacha kazi?”

”Efrazia hilo liache tu kama una swali lingine uliza?”

“Sina zaidi ya hilo.”

“Basi kama huna lingine tuendelee na mengine.”

“Rose njoo upate dawa ya kiuno mara moja nakuona unalalamika sana,” mzee Sionjwi  alisema baada ya kutoka bafuni kuoga.

“Shoga baadaye, ila ukiondoka usiache kuniaga.”

“Kwani dawa gani tena hiyo ya kukulaza?”

“Mmh, we mkubwa sasa si kila kitu uambiwe, hana dawa nyingine mzee anapenda kama chakula.”

“Na hilo tumbo hiyo dawa atakupaje.”

“Si ndo nakwambia yule mzee mwanga, baadaye mengine niachie mwenyewe usije ng’ang’ania bure usirudi mjini.”

Nilimuacha Rose akapate dawa ya kiuno japo nilikisia lakini sikuwa na uhakika na dawa ya kiuno huenda sivyo nilivyodhani. Kwa kweli ilichukua muda toka saa tisa mpaka saa kumi na mbili bado walikuwa hawajatoka. Nilijua lazima nilale na huenda kazi ikafanyika usiku.

Wasiwasi uliniingia huenda nami nikahamia kijijini kwa mzee Sionjwi, kama aliweza kunitembelea usingizini na kunipatia ujauzito lazima atataka kunibakiza nami kijijini. Mmh, woga uliniingia na kutamani niondoke bila kuaga. Lakini bado nisingefanya kitu kama Rose alirudi mjini na kumkuta kwa mzee Sionjwi hata mimi sikuwa na ujanja.

Lakini kuna kitu kilinipa moyo kutokana na pesa na misaada mingi niliyokuwa nampa lazima atauona umuhimu wangu wa kuniacha niendelee na kazi. Vilevile hata kama ningekimbia bado nafasi ya kwenda nje kusoma ningeikosa na muda ulikuwa umebaki mchache sana kuteua jina la mtu wa kwenda kusoma nje, nilisikia kuna mtoto wa mkubwa ndiyo kaandaliwa.

Nilijikuta nikipoteza woga wote na kuwa tayari kwa lolote ili mradi nafasi ile niipate.

Nikiwa katikati ya mazungumzo na wake wa mzee Sionjwi ambao hawakuonekana kuathiriwa na maisha ya kijijini. Kila mmoja aliyafurahia maisha yake tena waliishi kwa adabu kubwa kama wanawake wote wangekuwa kama wake wa mzee Sionjwi basi nyumba nyingi zisingevunjika.

Lakini kama wanaume wote wangekuwa na tamaa kama mzee Sionjwi watu wangezikwa kila kukicha kwa ukimwi kwa tabia yake ya tamaa ya wanawake kibaya hata kinga kwake hakutaka kuitumia.

Muda wote nilivyowaangalia watoto wake na uwezo wa baba yao nilichanganyikiwa kabisa kwa kuamini watoto wale kupata elimu itakuwa kazi. Niliamini kabisa mzee Sionjwi hata darasa moja hakupitia, kama angekuwa na elimu hata ya darasa la nne basi angejua jinsi ya kupanga uzazi au kuwa na wanawake wengi na uwezo wake ni mdogo.

Nikiwa katikati ya dimbwi la mawazo nilimuona Rose kwa mbali akija huku akijikongoja kama mzee na kuja nilipokuwa nimekaa huku tumbo likimtangulia mbele. Alipofika nilipokuwa nimekaa alisema huku akikishika kiuno chake huku tumbo akilitanguliza kwa mbele.

“Vipi mwenzangu kiuno kimepona au ndio kakizidisha?” Nilimuuliza baada ya kujifikilia kukaa huku ameuma meno.

“Dada kimepona.”

“Sasa mbona upo hivyo?”

“Dada weee kikongwe yule anapenda sifa hiyo dawa hajui kama nina tumbo hapa nipo hoi.”

“Mmmh, pole.”

“Dada usinipe pole, nipe hongera.”

Itaendelea kwenye Risasi Mchanganyiko.

JIUNGE NA GLOBAL BREAKING NEWS!

Leave A Reply