The House of Favourite Newspapers

Niyonzima Aitabiria Makubwa Yanga SC

0

KIUNGO mchezeshaji wa zamani wa Yanga, Mnyarwanda Haruna Niyonzima amesifu usajili wa timu yake hiyo huku akiitabiria makubwa katika msimu ujao.

 

Mnyarwanda huyo aliyewahi kuichezea Simba, hivi karibuni aliachana na Yanga na kwenda kujiunga AS Kigali ya nchini huko.

 

Akizungumza na Championi Jumatatu, Niyonzima alisema kuwa kati ya usajili bora uliowahi kufanywa ndani ya misimu miwili nyuma huu ni bora zaidi.

 

Mnyarwanda huyo alisema kuwa usajili huo uliofanywa nusu ya wachezaji anafahamu uwezo wao ambao aliwahi kukutana nao katika michuano mbalimbali ya kimataifa akiwa na Yanga, timu ya taifa ya Rwanda.

 

Aliongeza kuwa kwa usajili huo uliofanywa, kama wachezaji wataelewana na kucheza pamoja, basi upo uwezekano mkubwa wa timu hiyo kufanya vizuri katika michuano ya kimataifa na Ligi Kuu Bara.

 

“Kati ya timu niliyocheza muda mrefu na mafanikio Tanzania, basi Yanga ni ambayo imeshindwa kuchukua ubingwa wa ligi kwa misimu miwili kutokana na kutokuwa na timu bora.

 

“Lakini ninaamini kwa msimu huu itafanya vizuri kwa kuchukua ubingwa pamoja na kufika mbali kimataifa.

“Lipo wazi wamefanya usajili bora ambao umeendana na ubora wa timu, ukiangalia nusu ya wachezaji wapya ambao wamesajiliwa nawafahamu,”alisema Niyonzima.Azam FC: Tunakwenda

 

WILBERT MOLANDI, Dar es Salaam

Leave A Reply