BENKI ya NMB imetoa msaada wa mabati 1,248 na madawati 62 kwa ajili ya Shule 5 za Sekondari na shule 3 za Msingi zote kutoka halmashauri za Mkoa wa Katavi ikiwa ni kusaidia kutatua changamoto anuai kwenye sekta ya elimu.
Msaada huo uliogharimu kiasi cha shilingi milioni 40 umekabidhiwa na Meneja wa NMB Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Straton Chilongola huku akisisitiza benki hiyo itaendelea kusaidia jamii katika sekta ya afya, elimu pamoja na majanga ikiwa ni kuchochea maendeleo kwa jamii.
Akipokea msaada huo, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Lilian Matinga aliishukuru Benki ya NMB kwa kuchangia maendeleo ikiwemo kuthamini sekta ya elimu kwa msaada huo wenye tija.
Awali akitoa taarifa, Afisa Elimu Taalum Sekondari Manispaa ya Mpanda, Raphael Mkupi amebinisha kuwa wanafunzi katika shule ya Sekondari Rungwa hulazimika kukaa wawiliwawili kwa kiti kimoja kutokana na kuwepo kwa upungufu wa viti zaidi ya 300.
Comments are closed.