The House of Favourite Newspapers

NMB YATOA MSAADA WA TISHETI 250 KWA JESHI LA MAGEREZA

Afisa Mkuu Mkaguzi wa Ndani wa Benki ya NMB, Juma Kimori (kushoto) akimkabidhi msaada wa flana 250 Kamishna Msaaidizi Mwandamizi wa Magereza (SACP), Bertha Mende (kulia) kwa ajili ya wanamichezo wa Jeshi la Magereza Tanzania.
Afisa Mkuu Mkaguzi wa Ndani wa Benki ya NMB, Juma Kimori akizungumza kabla ya kukabidhi msaada wa flana 250 kwa ajili ya wanamichezo wa Jeshi la Magereza Tanzania. 
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza (SACP), Bertha Mende (katikati) akizungumza kuishukuru Benki yaa NMB kwa msaada wa flana ulizozitoa kwa wanamichezo wa Jeshi la Magereza nchini. 
Picha ya pamoja mara baada ya hafla ya makabidhiano kwa pande zote mbili.
Baadhi ya wageni waalikwa na wafanyakazi wa NMB wakishuhudia tukio hilo.

 

 

BENKI ya NMB imekabidhi msaada wa flana 250 kwa ajili ya wanamichezo wa Jeshi la Magereza Tanzania ambao wanaenda Zanzibar kushiriki kongamano la michezo.

 

 

Akizungumza wakati akikabidhi msaada huo, Afisa Mkuu Mkaguzi wa Ndani wa Benki ya NMB, Juma Kimori alisema ushirikiano mzuri wanaoupata kutoka kwa Jeshi la Magereza kibiashara kama wateja wao unawasukuma kushirikiana kila linapotokea jambo linaloitaji kushirikiana.

 

 

Aliwashukuru Jeshi la Magereza kwa kuwaamini na kuendelea kufanya kazi pamoja na kuwaomba kudumisha ushirikiano huo.

 

Kwa upande wake mwakilishi wa Jeshi la Magereza, akipokea msaada huo, Kamishna Msaaidizi Mwandamizi wa Magereza (SACP), Bertha Mende alisema wanafarijika kuona mara zote wanapoitaji ushirikiano na NMB wanawaunga mkono hivyo kuwahakikishia wataendelea kudumisha. Alisema NMB imekuwa ikiwasaindia mambo mengi bila kuchoka na kuwaomba waendeleze uhusiano huo.

Comments are closed.