The House of Favourite Newspapers

Obama Ashutumu Ukatili wa Kutenganisha Familia

RAIS mstaafu wa Marekani Barack Obama aliitumia Siku ya Wakimbizi Duniani kumshutumu Rais wa Marekani,   Donald Trump  katika sera yake ya kuwatenganisha watoto na familia zao.

Obama aliyasema hayo kupitia mtandao wa Facebook akiuliza iwapo Marekani inakubali ukatili wa kuwatengenisha watoto na wazazi wao.

Aliongeza kwamba: “Tuthibitishe kupitia sera, sheria na vitendo vyetu kwamba tunathamini familia zetu na zingine zote.”

Former President Barack Obama used World Refugee Day to criticize President Donald Trump's policy of separating migrant children and families

Obama.

Rais Trump amekuwa akiendesha sera ya kuwatenganisha watoto wakimbizi na familia zao hasa wale wanaoingia Marekani, hili limo katika amri aliyosaini karibuni.

President Trump signed an executive order on Wednesday reversing the separation policy

Katika sera ya Trump, utawala wake umewatenganisha watoto 1,995 kutoka kwa wazazi wao 1,940 tangu Aprili hadi Mei 31 mwaka huu kufuatia matukio mbalimbali, yakiwemo ya uhamiaji.

Comments are closed.