Omotola ashinda tuzo za Mwanamke Mburudishaji
NYOTA wa filamu wa Nigeria (Nollywood) Omotola Jalade-Ekeinde, hivi karibuni ameshinda tuzo inayotolewa na wanahabari ya Mwanamke Mburudishaji (Female Entertainment Personality).
Mcheza sinema huyo maarufu, mke wa Kapteni Ekeinde, na ambaye hivi karubuni alikuwa amelazwa hospitali, huku akihudumiwa na mumewe huyo, alipata zawadi hiyo iliyompa nafuu kubwa baada ya kutoka hospitalini.