The House of Favourite Newspapers

Onyango Akabidhiwa Tuzo Simba SC

0

BEKI kisiki wa Simba raia wa Kenya, Joash Onyango, amekabidhiwa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwezi Machi wa kikosi hicho baada ya kupigiwa kura nyingi na mashabiki.

 

Onyango amewashinda Aishi Manula na Luis Miquisone kwenye kinyang’anyiro hicho cha kuwania tuzo hiyo inayodhaminiwa na Kampuni ya Emirates Aluminium Profi le.

Beki huyo anakuwa mchezaji wa pili kutwaa tuzo hiyo iliyoanza kutolewa Februari, mwaka huu na kubebwa na Luis. Mbali na kupewa tuzo, Onyango amekabidhiwa kitita cha shilingi milioni moja.

 

Akizungum za baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo jana Jumatatu kwenye mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika Simba Mo Arena, Dar, Onyango alisema: “Tuzo hii itaongeza morali kwangu na kwa wenzangu katika hali ya kuendelea kupambana kwa ajili ya miezi mingine ijayo.

 

Kwa upande wa Ofi sa Mahusiano wa Emirates, Issa Maeda, amesema: “Tutaendelea kutoa tuzo hizi hadi mwisho wa msimu, mambo yakiendelea kuwa mazuri, msimu ujao tunaweza kuwepo tena na kuongeza dau kufi kia shilingi milioni tano.

 

WAANDISHI: MUSA MATEJA, LEEN ESSAU NA HAWA ABOUBAKHARI

Leave A Reply