The House of Favourite Newspapers
gunners X

Pablo Aanza na Kagere, Mugalu

0

SHAUKU ya kupata mabao ya Kocha Mkuu wa Simba raia wa Hispania, Pablo Franco, imemfanya aanze kuitengeneza safu ya ushambuliaji kati ya Meddie Kagere na Chris Mugalu, ili waweze kucheza kwa pamoja katika mechi yao dhidi ya Prisons itayopigwa leo.

 

Simba ipo nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara, ikiwa na pointi 25, iliyozikusanya katika michezo 13, ambapo imeshinda saba, sare nne na kufungwa miwili.


Chanzo chetu kutoka Simba,
kimeliambia Championi Jumatano kwamba, pamoja na timu hiyo kufuzu hatua ya 16 Bora ya Kombe la Shirikisho la Azam Sports, dhidi ya Dar City kwa ushindi mnono wa mabao 6-0, ambapo Kagere alifunga mabao mawili na Mugalu moja, tayari kocha Pablo ameonekana kuwanoa Kagere na Mugalu ili wacheze pamoja dhidi ya Prisons.


“Kelele za mashabiki wa Simba juu
ya straika wetu kutofunga kwenye ligi, nadhani tayari kocha Pablo ameamua kuzinyamazisha, ambapo katika mazoezi ya kwanza tu, ameonekana kuwahimiza Kagere na Mugalu kucheza kwa ushirikiano ili atakapowapatia nafasi ya kuanza pamoja basi waweze kufunga mabao mengi.


“Kocha Pablo nadhani anafanya hivyo
baada ya kuona furaha ya mashabiki zetu, baada ya kuvuna ushindi mnene dhidi ya Dar City, hivyo ameamua kuhakikisha hasira za kutopata bao anazipeleka katika mchezo wetu wa Ijumaa hii dhidi ya Prisons,” kilisema chanzo hicho.


Kwa upande wake Pablo alisema: “Safu
ya ushambuliaji bado imekuwa na umakini mdogo katika eneo la ufungaji kwa sababu bado imekuwa ikikosa nafasi nyingi za kufunga mabao kadiri muda wa mchezo unavyokwenda kitu ambacho naamini siyo kizuri kwa upande wetu kutokana na changamoto kubwa ambayo ipo mbele yetu.”

Musa Mateja na Ibrahim Mussa

Leave A Reply