The House of Favourite Newspapers

Pacha wa Manara azua taharuki uwanjani

0

DUNIANI wawili, hilo lilionekana dhahiri kwa shabiki wa Yanga ambaye alikuwa anafanana kila kitu na msemaji wa Simba Haji Manara.

 

Jamaa huyo ambaye anatambulika kwa jina la Injinia yupo kila kitu kama Manara. Mashabiki wa Yanga na wale wa Simba walionekana kuduwaza na muonekano wa jamaa huyo ambaye alionekana ni mtu mwenye pesa nyingi.

 

Akizungumza na Championi Jumatatu Injinia alisema: “Mimi sitaki kuzungumzia Manara hapa, ingawa najua yeye ni Yanga damu kabisa na yupo Simba kwa ajili ya maslahi yake na maisha binafsi.

 

“Mimi ni Injinia na yeye ni Manara hivyo watu wasitufananishe kabisa.”

ISSA LIPONDA, Dar es Salaam

Leave A Reply