Paul Pogba na PSG Mambo Yamenoga
WAKALA wa staa wa Manchester United, Paul Pogba, Mino Raiola yupo kwenye majadiliano na Paris Saint-Germain kwa ajili ya usajili wa mteja wake huyo huko wakimtaka kwa pauni 43m.
Pogba amesaliwa na mkataba wa mwaka mmoja ndani ya Man United na bado hajafanya mazungumzo na klabu yake ya sasa.
Si mara ya kwanza kwa kiungo huyo kutaka kuondoka ndani ya United na safari hii huenda akaondoka kikosini hapo.
PSG wanaamini kuwa wanaweza kumpata Pogba kwa pauni 43m ndiyo maana imeelezwa kuwa kwa sasa hivi wako kwenye mpango wa kuwauza baadhi ya nyota wa kikosi hicho ilikuweza kupata pauni 50m za usajili wake.
Taarifa zinaeleza kuwa PSG wanaomba kupunguziwa bei katika kumpata nyota huyo wa Man United.
Hata hivyo, Man United awali ilieza kuwa nyota wake huyo watafanya naye mazungumzo baada ya michuano ya Euro 2020 kwa ajili ya mkataba mpya, lakini mpaka sasa kumekuwa kimya na haijafahamika kama atasalia hapo au ataondoka.
PARIS, Ufaransa