The House of Favourite Newspapers

Pawasa Adai Ligi ya Soka la Ufukweni Itasimama Kupisha Dirisha la Usajili

0
Ligi ya soka la Ufukweni ikiendelea katika fukwe ya Coco

MRATIBUwa Soka la Ufukweni Bohiphace Pawasa amesema kesho mechi za kundi A zitakamilisha hatua za makundi na baada ya hapo ligi itasimama kwa muda wa wiki mbili ili kupisha kipindi cha dirisha la usajili.

Mratibu wa Ligi ya Soka la Ufukweni Boniface Pawasa amesema kuwa mashabiki waendelee kujitokeza kushuhudia ushindani mkubwa unaoendelea kwenye ligi hiyo.

Pawasa amedai baada ya dirisha la usajili kufungwa ligi ya ufukweni itarejea tena katika hatua ya robo fainali kwani michezo ya kesho itakamilisha ratiba kwani tayari timu 8 zimeshapatikana na zitajiandaa kwa ajili ya hatua ya robo fainali ya Ligi hiyo.

Leave A Reply