Punde baada ya kupokea habari ya kifo cha ghafla cha gwiji wa muziki wa Soukus Papa Wemba akiwa katika tamasha la muziki la Abidjan Ivory Coast , maelfu ya jamaa marafiki na mashabiki wake walianza kumiminika nyumbani kwake huko Kinshasa katika jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.