The House of Favourite Newspapers

Picha: Nandy na Aslay Wafanya Makamuzi Ya Nguvu Escape One, Mikocheni

Nandy na Aslay wakifanya yao Usiku wa kuamkia leo Escape One Masaki.
Msanii wa Bongo Fleva, Faustina Charles ‘Nandy’ akitoa burudani.

ULIKUWA ni usiku wa shoo kabambe kutoka kwa wasanii wanaofanya vizuri na ngoma yao ya ‘Subalkher’ ambao ni Nandy na Aslay. Shoo hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Escape One, Mikocheni jijini Dar es Salaam ambayo ilikuwa iliandaliwa maalum kwa ajili ya kusheherekea Siku ya Wapendanao (Valentine Day).

 

Mashabiki waliburudika kwa wasanii hao kwa kila mmoja kuimba ngoma zake na baadaye wakaziamsha hisia za wapendanao waliofika ukumbini hapo kwa kuimba kwa pamoja wimbo wao yenye ujumbe mzito wa mapenzi wa ‘Subalkher’.

 

Wakati akipafomu wimbo wake wa ‘Mama’, Aslay, alizigusa hisia za mashabiki waliofika ukumbini hapo akiwemo mama wa msanii Nandy ambaye alionekana kutamani kulia kutokana na maneno aliyokuwa akiongea Aslay ya kuelezea uchungu alionao juu ya kifo cha mama yake mzazi.

(PICHA: MUSA MATEJA | GLOBAL PUBLISHERS)

Comments are closed.