IKIWA ni mwezi mtukufu wa toba kwa waumini wa Dini ya Kiislam ambao kwa sasa wapo kwenye mfungo duniani kote, wakali wa burudani jijini Dar Es Salaam, Maisha Basement jana walialika watu kibao kwa nia ya kula nao futari ya jioni kuonyesha ukarimu wao kwa jamii inayowazunguka.
Futru hiyo ilifanyika katika Ofisi za Ester Entertainment ambao ni wamiliki wa Maisha Basement zilizopo Mwananyamala jijini Dar huku wasanii kibao wakijitokeza katika mjumuiko huo.
PICHA NA MUSA MATEJA | GLOBAL PUBLISHERS