MWILI wa aliyekuwa shabiki maarufu ya Klabu ya Yanga, Ally Mohammed maarufu kama Ali Yanga jana uliagwa wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma na kusafirishwa kwenda kuzikwa kwao mkoani Shinyanga.
Miongoni mwa waliohudhuria tukio hilo la kumuaga Ali, ni pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Jordan Rugimbana na Waziri wa zamani wa Habari na Michezo, Nape Nnauye, mashabiki na wanachama wa Yanga na wapenda soka.
Ali Yanga alifariki juzi Jumatatu, Mpwapwa, Dodoma kwa ajali ya gari ambapo baada ya kuagwa jana mwili wake ulisafirishwa kwenda kwao Shinyanga kwa mazishi ambayo yanafanyika leo.