MBUNGE wa Mtama, mkoani Lindi kwa Tiketi ya CCM, Nape Nnauye leo Machi 25, 2017 ameamsha shangwe kwenye Uwanja wa Taifa wakati wa mechi kati ya Taifa Stars na Botswana.
Nape alinyanyuka kuwasalimia mashabiki wa Taifa Stars wakati wa kipindi cha mapumziko kwenye mchezo huo, jambo lililowashangaza wengi na kuanza kumshangilia kwa nguvu huku wakipiga makelele za kuimba Nape… Nape…. Nape!.
Pamoja na kumshangilia, wengi walikuwa wakigongana kutaka kupiga naye picha naye aliwapa nafasi mashabiki hao.
Baadaye Nape alionekana akiwa ameketi na kupiga stori na Waziri wa habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt, Harrison Mwakyembe ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mchezo huo. Nape ambaye nafasi yake aliteuliwa Mwakyembe juzi Alhamisi, amekuwa gumzo kwenye mitandao ya kijamii siku za hivi karibuni.
Comments are closed.