The House of Favourite Newspapers

Pikipiki ya 4 Yakabidhiwa, Mume, Mke Wageuka Kivutio Tusua Maisha na Global

Abbas Shekwavi (kushoto) anayemwakilisha mshindi wa pikipiki kutoka Dodoma, Hassan Shekwavi akikabidhiwa funguo na kadi ya pikipiki na Erick Evarist, Mhariri wa Gazeti la Amani.

Hatimaye washindi wa droo ya nne ya tusua maisha na Global, wamekabidhiwa zawadi zao Ijumaa katika Ofisi za Global Publishers, Sinza Mori jijini Dar es Salaam ambapo wanandoa Asha Kombo na mumewe, Omary Kisigalile wamegeuka kivutio wakati wakikabidhiwa zawadi.

Abbas Shekwazi akiwa amepanda pikipiki aliyokabidhiwa kwa niaba ya kaka yake, Hassan Shekwavi.

Asha aliyebuka mshindi wa ada ya shule katika droo iliyochezeshwa mubashara kupitia Global TV Online, amefika katika ofisi za Global akiwa ameambatana na mumewe  na alipopewa nafasi ya kuzungumza chochote baada ya kukabidhiwa zawadi hiyo, alianza kwa kumshukuru mumewe kwa jinsi anavyomjali, kiasi cha kuacha kazi zake zote na kumsindikiza kupokea zawadi.

Mshindi wa ada ya shule, Asha Kombo akiwa na mumewe, Omary Kisigalile mara baada ya kukabidhiwa zawadi yao.

“Mume wangu ameniwekea bili ya magazeti, mimi kila siku naletewa magazeti mpaka mlangoni na gazeti ninalolipenda zaidi niIjumaa, yeye huwa anasoma Championi, kwa hiyo hata huu ushindi wa leo, ni kwa ajili yake,” alisema Asha na kuongeza kwamba ada aliyoshinda, atamlipia mwanaye anayesoma kidato cha kwanza na kumnunuliamahitaji, lakini pia atamlipia mwanaye mwingine anayesoma shule ya kulipia.

Aziz Hashim (katikati), mwakilishi wa Kampuni ya Global Publishers akizungumza wakati wa zoezi la kuwakabidhi zawadi washindi. Wengine ni John Joseph, mwakilishi wa Sokabet na Glory Lucas kutoka Idara ya Uhasibu Global Publishers.

“Unajua siku hizi sawa wanasema elimu bure lakini kuna mahitaji muhimu ambayo ni lazima uwe na fedha, nawashukuru sana Global kwa hiki mlichokifanya, Mungu awabariki sana.

Asha Kombo, akifurahia ada ya shule aliyojishindia kupitia Tusua Maisha na Global.

Naye Abbas Shekwavi ambaye amemwakilisha mshindi wa pikipiki, Hassan Shekwavi kutoka Dodoma, amesema awali alikuwa haamini kama ni kweli mtu yeyote anaweza kuwa mshindi lakini baada ya kushuhudia kaka yake akiibuka na pikipiki mpya, atakuwa balozi mzuri wa kuwaelimisha wengine.

 

“Ndugu yangu ni mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Tambukareli, Dodoma na hana mtu yeyote anayefahamiananaye hapa Global, niliposikia ameshinda na leo nakabidhiwa zawadi kwa niaba yake, kwa kweli nimefarijika sana ndani ya moyo wangu na namuomba Mungu awabariki viongozi na wafanyakazi wote wa Global. Kazi mnayoifanya ni kubwa sana.

 

Mwingine ambaye alipaswa kukabidhiwa zawadi yake leo, ni Mary Mwalingo wa Mbeya ambaye hakuwa na mwakilishi hapa jijini Dar es Salaam, hivyo ameshindwa kuhudhuria zoezi la kupokea zawadi lakini atatumiwa zawadi yake ya dinner set na kukabidhiwa na wakala wetu mkoani Mbeya.

Comments are closed.